Saturday 25 May 2013

NUSURA KUCHOMWA MOTO KISA 350,000 MANGO GARDEN (KINONDONI) DAR

(Mchunguzi wetu kutoka  Dar): Majira ya saa 9:00 alasiri, katika Ukumbi wa Mango Garden, Kinondoni jijini Dar es Salaam, kijana mmoja (poichani) alikurupushwa kwa kupigiwa kelele za 'mwizi' na mtu aliyedai kutapeliwa naye. Wananchi walianza kumkimbiza hadi walipogotea maeneo ya Vijana, Kinondoni baada ya mtuhumiwa kujikwaa na kuanguka. Baada ya adayedaiwa kutapeliwa kuwafahamisha mkasa wa kutapeliwa shilingi 350,000/-, wananchi walimpekua 
mtuhumiwa na kukutwa na makaratasi yaliyokatwa na kufungwa kwa noti bandia za shilingi elfu kumi, vitambulisho vya watu mbalimbali kama vile leseni, picha za pasipoti, barua za serikali za mitaa za jijini Dar es Salaam n.k. Alipoulizwa kuwa vitu hivyo vya watu na nyaraka za serikali ni vya nini au alivipataje, jamaa huyo alijitetea kuwa ana mtu anayeshirikiana naye katika shughuli hiyo. Salama yake ya kutokuuawa na kuachwa akiwa katika hali mbaya, ilikuja baada ya madereva wa taxi wa eneo hilo kusema hawataki kuachiwa ushahidi wa kuchoma moto mtu huyo katika eneo lao. 

0 comments: