Monday 27 May 2013

MTOTO MCHANGA WA SIKU 4 AKAA NDANI YA SHIMO SIKU 6 AKIWA HAI

HUYU NDO MTOTO MCHANGA WA SIKU 4 ALIYEKAA NDANI YA SHIMO SIKU 6 AKIWA HAI


Ndugu yangu ukishangaa ya Mussa basi shangaa na ya Filauni, Methali hiii methibitika Songea baada ya Mtoto Bahati Upendo mwenye siku 3 toka azaliwe alipo wekwa na mama yake kwenye mfuko wa mbolea na kutumbukizwa kwenye shimo...
 
Ndani ya shimo hilo amekaa siku 6 bila kula wala kunywa hadi alipo okotwa na wasamalia wema...
Hivi sasa yuko Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma akiwa Salama  Salimini .
Yeyote Mwenye nafasi ya kumsaidia mtoto huyu anaweza kwenda moja kwa moja Hospitali au wasiliana na namba zifuatayo,  mchango  utafuatwa 0755061588 au 0755 731 234.
Dawati la Police Wanawake Mkoa wa Ruvuma wakiwa na Wauguzi kuangalia usalama wa Mtoto huyo aliye Tupwa. Kutoka kulia ni Muguzi Rukia Twahili anaye fuata Devota Umbela na aliye mshika mtoto Mwenyekiti wa Mtandao wa Police Wanawake Fadhila Chacha na wa mwisho kushoto ni A nna Chaima 

0 comments: