Wednesday, 16 July 2014

CHELSEA YAMNASA FILIPE LUIS, DEMBA BA KWENDA UTURUKI,

 
CHELSEA YAMCHUKUA BEKI FILIPE LUIS TOKA ATLETICO MADRID
FILIPE-LUISChelsea wamekubaliana na Mabingwa wa Spain Atletico Madrid kumnunua Beki wa Kushoto anaetoka Brazil Filipe Luis.
Mchezaji huyo mwenye Miaka 28 sasa atakwenda Stamford Bridge kwa upimwaji afya yake na kumalizana kuhusu maslahi yake binafsi.
Msimu uliopita, Luis alichezea Atletico Mechi 44 na kuwasaidia kutwaa Ubingwa wa La Liga na kufika Fainali ya UEFA CHAMPIONZ LIGI waliyopigwa 4-1 na Real Madrid.
Luis anakuwa Mchezaji wa Pili wa Atletico kusaini kuichezea Chelsea kufuatia Straika Diego Costa nae kujiunga.
Beki huyo, ambae amekuja kuchukua Namba ya Ashley Cole aliekataliwa kuongezewa Mkataba na kutimkia AS Roma ya Italy, alijiunga na Atletico Mwaka 2010 akitokea Deportivo La Coruna.
Luis ameichezea Brazil mara 4 na aliwekwa kwenye Kikosi cha Akiba cha Brazil kwa ajili ya Fainali za Kombe la Dunia zilizoisha hivi Juzi.
SASA BARCA YASEMA LUIS SUAREZ NI WAO!SUAREZ
Barcelona imesema Straika wa Liverpool Luis Suarez ni Mchezaji wao kwa Asilimia Mia Moja.
Wiki iliyopita Liverpool na Barca zilikubaliana Dili ya Pauni Milioni 75 ya Uhamisho wa Mchezaji huyo mwenye Miaka 27 kutoka Uruguay.
Lakini Barca hawaruhusiwi kumtambulisha rasmi Mchezaji huyo kwa vile yuko kwenye Kifungo cha Miezi Minne kutojihusisha na shughuli yeyote ya Kisoka baada kupatikana na hatia ya kumuuma Meno Beki wa Italy Chiellini wakati wa Mechi ya Kombe la Dunia kati ya Uruguay na Italy huko Brazil.
DEMBA_BA-AENDA_CHELSEAMkurugenzi wa Michezo wa Barca, Andoni Zubizarreta, amewaambia Wanahabari kuwa Suarez sasa ni Mchezaji wao kwa Asilimia 100.
Amesema: “Tunawakubali Watu hapa na kasoro zao zote. Nina hakika atakuwa Mtu wa mchango mkubwa kwetu. Ni Mchezaji muhimu.”
DEMBA BA: BESIKTAS WAONGEA NA CHELSEA ILI KUMSAINI!
Klabu ya Uturuki Besiktas imetoboa kuwa ipo kwenye mazungumzo na Chelsea ili wamsaini Straika kutoka Senegal Demba Ba.
Ba, mwenye Miaka 29, alianza Mechi 23 kati ya 50 alizochezea Chelsea Msimu uliopita na kufunga Bao 14.
Kwenye Msimu huo, Ba alikuwa nyuma kwa namba akiwa chaguo la mwisho baada ya Samuel Eto'o na Fernando Torres.
Lakini Eto’o hivi sasa amemaliza Mkataba na Chelsea wamemsaini Diego Costa na hivyo Ba kuonekana hahitaji 

Related Posts:

0 comments: