Sunday, 13 July 2014

LIONEL MESSI MCHEZAJI BORA KOMBE LA DUNIA 2014,NEUER KIPA BORA


LIONEL Messi amepoza machungu kidogo baada ya kushinda tuzo ya mchezaji bora wa Kombe la Dunia 2014. Nyota huyo wa Barcelona ameshindwa kuisaidia Argentina kutwaa Kombe la Dunia baada ya kufungwa 1-0 na Ujerumani katika Fainali  Uwanja wa Maracana mjini Rio de Jeneiro, Brazil.   Bao hilo pekee la Ujerumani, lilifungwa na Mario Gotze aliyeingia kuchukua nafasi ya Miroslav Klose dakika 88, aliyefunga bao hilo pekee dakika ya 112.
  Mlinda mlango wa Ujerumani, Manuel Neuer ameshinda tuzo ya kipa bora wa mashindano ya mwaka huu, ambayo wenyeji Brazil wameambulia nafasi ya nne baada ya kufungwa 3-0 na Uholanzi jana, kufuatia kutolewa na Ujerumani kwa kipigo cha mabao 7-1 katika Nusu Fainali. James Rodriguez wa Colombia amekuwa mfungaji bora kwa mabao yake sita, licha ya timu yake kutolewa Robo Fainali. Amefuatiwa na Thomas Muller wa Ujerumani mabao matano, Lionel Messi mabao manne sawa na Robin van Persie wa Uholanzi.

Related Posts:

0 comments: