Tuesday, 8 July 2014

DEBUCHY ATUA ARSENAL RASMI KWA AJILI YA VIPIMO

BEKI Mathieu Debuchy yuko mbioni kukamilisha uhamisho wake wa Pauni Milioni 11 kutua Arsenal akitoka kwa wapinzani wa Ligi Kuu ya England, Newcastle.
Beki huyo wa kulia wa Ufaransa amekuwa akihusishwa na kuhamia The Gunners kwa wiki kadhaa sasa na sasa anatarajiwa kusaini baada ya Fainali za Kombe la Dunia.
Ufaransa ilitolewa katika Robo Fainali na Ujerumani na Debuchy amerejea England kukamilisha vipimo vya afya na The Gunners Jumatatu.

Mshika Bunduki mpya? Debuchy yuko mbioni kukamilisha uhamisho wake Arsenal

Uamuzi wa Arsenal kumfuata Debuchy unafuatia kuondoka kwa Bacary Sagna anayehamia Manchester City kama mchezaji huru.
Debuchy alikuwa anaanzishwa mbele ya Sagna katika kikosi cha Ufaransa kwenye Kombe la Dunia. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 ameichezea mechi 46 Newcastle, akiifungia bao moja tu - dhidi ya wapinzani Sunderland.
Alisajiliwa kutoka Lille ya Ufaransa kwa Pauni Milioni 5.5 Januari mwaka 2013 na Newcastle sasa inataka kumsajili ama Micah Richards wa Manchester City au Carl Jenkinson wa Arsenal wazibe pengo la kisiki hicho.

Related Posts:

0 comments: