Monday, 7 July 2014

ARSENAL YAWEKA MEZANI PAUNI MILIONI 34 KUNUNUA SAINI YA SANCHEZ

KLABU ya Arsenal imekubali kutoa Pauni Milioni 34 kwa Barcelona ili kumnunua mshambuliaji wa kimataifa wa Chile, Alexis Sanchez ingawa Barca wanasubiri kuona kama Juventus nap watatoa kiwango kama hicho.

Sanchez ameonyesha hataki kuhamia Liverpool licha ya jitihada zao za kumshawishi aende kuungana na kikosi cha Brendan Rodgers. 
Hiyo inatokana na kwamba Liverpool nato imekubali kumuuza mshambuliaji wake, Luis Suarez kwa Barcelona.

Chaguo: Sanchez amegoma kwenda Liverpool

Manchester City pia wanamtaka mchezaji huyo na wake tayari kumrudisha Hispania mshambuliaji wao Alvaro Negredo.
Liverpool pia imetoa ofa ya Pauni Milioni 19.8 kwa ajili ya winga wa Benfica, Lazar Markovic na mazungumzo yanaendelea kwa ajili ya mshambuliaji wa Lille, Divock Origi kupitia wawakilishi wake nchini Brazil.
Juventus iko vibaya kiuchumi na inakabiliwa na mtihani wa kumzuia mshambuliaji wake Paul Pogba anayetakiwa na PSG na Manchester City.Way out? Juventus may have to sell Paul Pogba to raise money if they want to bid for Sanchez
Ataondoka? Juventus inaweza kumuuza Paul Pogba kuongeza fedha za kufika dau la Sanchez

Related Posts:

0 comments: