Baadhi ya waandishi wa habari wakichukua matukio
Na Denis Mlowe,Iringa
WANAHABARI mkoani
Iringa wametakiwa kufata weledi wa kazi zao kwa kuelimisha jamii kwa
kufanya kazi kulingana na maadili yao ya kazi na sio kwa maslahi ya
vyama au mtu binafsi.
Hayo yamesemwa na mbunge wa Iringa Mjini Mch Peter Msigwa
wakati akizungumza na wandishi wa habari ofisini kwake juzi kuwa
wanahabari wengi wamekuwa wakiandika habari ambazo zimekuwa hazina
maadili kwa hofu ya baadhi ya vyama au viongozi fulani kuwatisha.
Msigwa alisema kuwa baadhi ya wandishi wa habari wamekuwa wakizuiwa kuzungumza na mbunge wa Iringa mjini kutokana na kuwa yupo katika chama cha upinzani.
Hata hivyo msigwa alisema kuwa wandishi wanatakiwa kuondokana na dhana hiyo na kutokuogopa kauli wanazotishiwa kwa kutokufanya kazi na mtu au chama fulani kutokana na kuwa hakuna mtu aliye juu ya sheria.
Aidha ameongeza kwa kusema kuwa wandishi wanapaswa kuandika habari zilizo na ukweli lakini pia panapopaswa kukosolewa wasisite kukosoa hata kama anayekosolewa akiwa ni kiongozi wa aina gani.
Msigwa alisema kuwa baadhi ya wandishi wa habari wamekuwa wakizuiwa kuzungumza na mbunge wa Iringa mjini kutokana na kuwa yupo katika chama cha upinzani.
Hata hivyo msigwa alisema kuwa wandishi wanatakiwa kuondokana na dhana hiyo na kutokuogopa kauli wanazotishiwa kwa kutokufanya kazi na mtu au chama fulani kutokana na kuwa hakuna mtu aliye juu ya sheria.
Aidha ameongeza kwa kusema kuwa wandishi wanapaswa kuandika habari zilizo na ukweli lakini pia panapopaswa kukosolewa wasisite kukosoa hata kama anayekosolewa akiwa ni kiongozi wa aina gani.
Msigwa alisema kuwa kiongozi yoyote anayezuia watendaji wake kufanya kazi za jamii hajui utendaji wa kazi zake.
Aidha msigwa ameongeza kuwa viongozi wengi wanashindwa kujua
wajibu wao katika ngazi walizopo akiwemo katibu mkuu wa ccm mkoa wa
Iringa kuingilia kazi za madiwani.
0 comments:
Post a Comment