Sunday, 13 July 2014

PROF. MSOLA ATOA MSAADA WA MIPIRA KILOLO

SAM_6549 
Mbunge wa jimbo la Kilolo Prof. Peter Msola akimkabidhi mpira nahodha wa timu ya kijiji cha Mwatasi Inocent Myava. SAM_6518 
Mbunge wa jimbo la Kilolo Prof. Peter Msola akimkabidhi mpira nahodha wa timu ya kijiji cha Mwatasi kwa upande wa wanawake Angelina Ngusa.
Na Denis Mlowe,Kilolo
VIJIJI 6 vya jimbo la Kilolo katika wilaya ya Kilolo mkoani Iringa vimepata msaada wa mipira mitatu kila kimoja kwa wanaume na wanawake pamoja shule moja kwa kila kijiji kwa ajili ya kujiandaa na michezo mbalimbali inayotarajia kufanyika wilayni humo.
Vijiji vilivyofaidika na msaada huo ni kijiji cha Mwatasi, Mwangama, shule ya msingi Ng’ingula shule ya msingi Bomalang’ombe, Masisiwe, Nyawegeti na Isanga ikiwa na thamani ya sh. Laki tisa na nusu(9.5) zote za wilaya ya Kilolo.
Msaada huo ulitolewa juzi na mbunge wa jimbo la Kilolo,Prof. Peter Msola wakati akizungumza na wananchi wa kata Bomalang’ombe ikiwa ni utaratibu wake kuwatembelea wananchi na kusikiliza kero zao kwa lengo la kukuza soka na mchezo wa mpira wa mikono katika wilaya hiyo.
Akikabidhi msaada huo,Msola alisema michezo ina nafasi kubwa ya kuajiri vijana na ni jukumu la wadau kusaidia kukuza michezo yote na moja ya ahadi zake za kukuza michezo katika wilaya ya Kilolo wakati akitaka ridhaa ya wananchi wa jimbo hilo kuwakilisha kuwa mbunge wao.
Msola aliwaomba wananchi wa jimbo hilo kuwekeza katika michezo kutokana kwa sasa imekuwa ajira ambayo inawapatia kwa kiasi kikubwa maisha vijana na wale wote wanaoshiriki michezo kama ajira.
Aidha Pro. Msola aliwaahidi wanakazi wa kijiji cha Ng’ingula kuwapatia seti ya jezi mara baada ya nahodha wa timu ya kijiji hicho kumtaka mbunge huyo kuwapatia msaada wa jezi kutokana na kutokuwa nazo pindi ligi mbalimbali zinazoendeshwa jiimboni humo ikiwemo mashindano ya kombe la jimbo ambapo yanadhaminiwa na mbunge huo.

Related Posts:

0 comments: