Tuesday, 8 July 2014

MSHAHARA WA COLE WAPUNGUA PAUNI 160,000 KWA WIKI BAADA YA KUTUA AS ROMA YA ITALIA

MSHAHARA wa Ashley Cole umepungua kwa Pauni 160,000 kwa wiki baada ya kutua AS Roma ya Itali, kutoka Pauni 200,000 alizokuwa akilipwa Chelsea.
Cole alitua Italia jana na kusaini Mkataba wa miaka miwili kujiunga na timu hiyo ya Serie A kwa mshahara wa Pauni Milioni 1.8 kwa msimu (kiasi cha Pauni 35,000 kwa wiki).
Lakini mshahara wa mchezaji huyo unaweza kuongezeka hadi Pauni 80,000 kwa wiki kutokana na posho mbalimbali.

Maisha mapya: Cole aliwasili jana katika Uwanja wa mazoezi wa Roma na kusaini Mkataba wa miaka miwili 

Related Posts:

0 comments: