Monday, 16 June 2014

STAA ALIEIUA URUGUAY KURUDI ARSENAL, VERMAELEN KWENDA OLD TRAFFORD!



THOMAS_VERMAELENFOWADI wa Costa Rica Joel Campbell amethibitisha kuwa atarudi Arsenal baada ya kumalizika michuano ya Kombe la Dunia huko Brazil huku Nahodha wa Klabu hiyo, Thomas Vermaelen, akiripotiwa njiani kwenda Old Trafford..
FOWADI WA COSTA RICA JOEL CAMPBELL
Campbell hajawahi kuichezea Arsenal na kwa Misimu Mitatu sasa amekuwa nje kwa Mkopo tangu anunuliwe Agosti 2011 toka Klabu ya Saprissa.
Tangu wakati huo, Campbell amecheza kwa Mkopo kwenye Klabu za Lorient, Real Betis na Msimu uliokwisha Mwezi Mei alikuwa huko Ugiriki na Olympiakos.Joel_Campbell
Campbell, mwenye Miaka 21, Juzi alifunga Bao wakati Costa Rica ikiwagaragaza Uruguay kwa Bao 3-1 kwenye Mechi yao ya Kwanza ya Kundi D la Fainali za Kombe la Dunia huko Brazil.
Akiongea na Wanahabari, Kijana huyo alithibitisha: “Inabidi nirudi Arsenal, kwa sababu nina Mkataba nao. Lakini kwa sasa kitu muhimu ni Nchi yangu na Kombe la Dunia!”
Mechi inayofuata kwa Costa Rica ni dhidi ya Italy na mwisho watamaliza na England kwenye Kundi D.
Campbell amesema: “Haikutushangaza kuifunga Uruguay, tumekuja hapa kushinda. Ndio maana unacheza Kombe la Dunia!”
THOMAS VERMAELEN KUTUA MANCHESTER UNITED?
Nazo habari kutoka Uingereza zinadai kuwa Nahodha wa Arsenal Thomas Vermaelen
huenda akahamia Manchester United.
Imeripotiwa kuwa Vermaelen tayari ameshafikia makubaliano na Man United baada ya kupewa Nyongeza ya Mshahara ya Pauni 30,000 na kumfanya awe juu ya Pauni Laki 1 kwa Mwezi.
Inasadikiwa Arsene Wenger hana kipingamizi kwa Beki huyo kutoka Belgium kuhamia Old Trafford kwa vile Meneja huyo wa Arsenal chaguo lake la Masentahafu ni Laurent Koscielny na Per Mertesacker.
Inaaminika Arsenal watamuuza Vermaelen kwa vile amebakiza Mwaka mmoja kwenye Mkataba wake ikiwa Man United watalifikia Dau la Pauni Milioni 10 ambalo walimnunua kutoka Ajax Miaka mitano iliyopita.
Mweyewe Vermaelen anapenda kujiunga na Old Trafford ili aungane tena na Louis van Gaal, Meneja mpya wa Man United, ambae walikutana huko Ajax.

\
XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX
Stealing the show: Joel Campbell inspired Costa Rica to an impressive win over Uruguay on Saturday
 Joel Campbell aliisaidia Costa Rica kuibamiza  Uruguay siku ya jumamosi.
 
KOCHA Arsene Wenger yuko tayari kumpa fursa Joel Campbell ya kuichezea Asernal. Kocha huyo wa Asernal ambaye yupo mjini Porto Alegre kama mtangazaji wa Televisheni ya Ufaransa, jumapili jioni alishuhudia Ufaransa ikichapa Honduras maao 3-0.
 Lakini Wenger amethibitisha kuwa amepanga kumrudisha tena katika kikosi cha Asernal nyota huyo wa  Cost Rica ambaye alifanya kazi nzuri wakiizamisha Uruguay.
Kocha huyo mnamo mwaka 2011 alimtoa kwa mkopo nyota huyo mwenye miaka 21.
Who's the daddy? Campbell celebrates after scoring Costa Rica's equaliser early in the second half
Campbell akishangilia bao lake la kusawazisha

‘Hakika atarudi kwetu wakati wa maandalizi ya msimu," Wenger aliwaambia Sportsmail. "Ameimarika vizuri".
Wenger iliikosa mechi ya Costa Rica kwasababu alisafiri kwenda Porto Alegre, lakini alipokea ujumbe kutoka kwa kocha wa zamani wa Chelsea Avram Grant, ambye yuko na luninga ya Israel akimtaarifu jinsi ambavyo Campbell alicheza vizuri.
Campbell aliifungia Costa Rica bao moja na kutengeneza nafsi moja katika ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Uruguay mjin Fortaleza.
Campbell alisaini mkataba na Asernal miaka mitatu iliyopita, lakini muda mrefu amecheza kwa mkopo , lakini Wenger anahisi sasa imefika muda muafaka wa kumrudisha katika timu ya kwanza ya klabu yake.
 Mara ya kwanza alipelekwa kwa mkopo katika klabu ya Lorient nchini Ufaransa, halafu Real Betis nchini Hispania na  kwasasa anaichezea timu ya Ugiriki ya  Olympiacos, ambapo amewavutia  Manchester United katika michuano ya ligi ya mabingwa.

Related Posts:

0 comments: