Tuesday, 8 July 2014

WAMBURA v/s SIMBA, NANI BINGWA? soma hapa


SIMBA-MICHAEL_WAMBURAMICHAEL WAMBURA ameendelea ‘vita’ yake na Klabu ya Simba baada ya kuwaonyaEVANS_AVEVAViongozi wapya wa Simba wakiongozwa na Rais Evans Aveva kwamba wanapaswa kuwasikiliza yeye pamoja na Wanachama 69 waliowasimamisha.
Juzi Kamati Kuu ya Simba, chini ya Rais Aveva, ikifanya Kikao chake cha kwanza, iliamua kuwasimamisha Wanachama 69 ambao waliwasilisha Kesi Mahakamani kutaka kusimamisha Uchaguzi Mkuu na pia kusema uamuzi wa hatima yao pamoja na ya Michael Wambura, aliezuiwa kugombea kwenye Uchaguzi huo, utatolewa na Mkutano Mkuu wa Simba utakaofanyika Agosti 3.
Lakini sasa Wambura ameibuka na kudai Wanachama hao wana hoja na ndio maana wakaenda Mahakamani na kuruhusiwa kufungua Shauri lao na hivyo Klabu inapaswa kuwasikiliza.
Wambura alikariri Ibara ya 41 (d) ya Katiba ya Simba aliyodai inataka Wanachama hao kuitwa na kupewa fursa ya kujitetea kabla hatua au uamuzi wowote kuchukuliwa dhidi yao.
Kuhusu yeye binafsi, Wambura amedai yeye suala lake lilimalizwa na TFF kupitia Kamati ya Rufaa ya Uchaguzi chini ya Mwenyekiti Julius Lugaziya ambayo ilimrudisha kwenye Uchaguzi Simba.
Wambura alieleza kuwa yeye ameshasafishwa na Kamati ya Lugaziya na ndio mana alirudishwa kwenye Uchaguzi huo na kuondolewa tu kwa sababu ya kosa la kufanya kampeni kabla muda na si vinginevyo na hivyo haoni mantiki ya yeye kupelekwa kwenye Mkutano Mkuu wa Agosti 3.
Hata hivyo, kiini cha zogo hili la Wambura na Simba inadaiwa ni uhalali wake wa kuwa Mwanachama hai.
Vile vile, Wambura alizungumzia Uchaguzi wa Simba uliofanyika Bwalo la Maafisa wa Polisi, Oyster Bay, Jijini Dar es Salaam hapo Juni 29 na kudai Wanachama wengi hawakuridhishwa na uendeshwaji wake na hivyo hawakubali matokeo.
Wambura alikumbusha kuwa wakati wa Mkutano huo wa Wanachama wa Uchaguzi, walitangaziwa kuwa idadi ya Wanachama waliohudhuria ni 2500 lakini kwa upande wa Uchaguzi wa Rais Kura zilizopigwa zilikuwa 1845 tu ikimaanisha Watu 700 hawakupiga Kura na hilo limezua shaka na kuibua uhalali wa Uchaguzi huo.
Kwenye Uchaguzi huo, Aveva alitinga madarakani baada ya kuzoa Kura 1455 na kumshinda Andrew Tupa aliepata Kura 388.
KAA CHONJO….sakata linaendelea….

Related Posts:

0 comments: