Monday, 7 July 2014

MATTHAUS: GUARDIOLA AMEKUWA NA USHAWISHI KATIKA SOKA LA UJERUMANI


Matthaus: Guardiola has influenced Germany
NAHODHA wa zamani wa Ujerumani, Lothar Matthaus anaamini Pep Guardioala ameingiza sumu zake kwenye timu ya taifa kwasababu kuna wachezaji wengi wa Bayern Munich.

Kocha huyo wa zamani wa Barcelona alianza kazi Bayern tangu majira ya kiangazi mwaka 2013 na kuiongoza klabu hiyo kutwaa makombe mawili ya nyumbani katika msimu wake wa kwanza.

Matthaus anaamini falsafa ya mpira wa Hispania imeingia katika wachezaji na kuanza kufanya kazi kwenye timu ya taifa wakitokea katika klabu yao ya Bayern Munich.

“Ni kweli kwamba Guardiola amekuwa na ushawashi fulani katika timu yetu. Inahusisha wachezaji wengi wa Bayern na wameanza kuleta staili yao ya mpira”. Alisema.

“Guardiola alishinda mataji mengi sana akiwa Barcelona na alikuwa na mafanikio makubwa. Alichukua baadhi ya falsafa za Barcelona na kuja nazo Bayern, na kwa vile Ujerumani ina wachezaji wengi wa Bayern, kumekuwepo na elementi za Guardiola katika timu”.

Matthaus alibeba kombe la dunia akiwa nahodha mwaka 1990- na mpaka sasa hakuna nahodha yeyote wa Ujerumani aliyefanikifiwa kupata mafanikio hayo.
Pia anashikilia rekodi ya kucheza mechi nyingi za kombe la dunia akiwa alicheza mechi 25.
Japokuwa  kikosi cha Joachim Low kinajulikana kwa kucheza soka la kuvutia, Matthaus amekiri kuwa timu hiyo kwasasa imebadilika na kucheza mpira wa nguvu utakaowasaidia kupata mafanikio katika fainali yao ya nne mfululizo ya kombe la dunia.

“Kushinda ndio kitu cha msingi zaidi katika fainali za kombe la dunia. Tumetumia miaka nane kucheza soka la mvuto, soka la ufundi, kwa staili ambayo hakuna aliyeijua Ujerumani na ilipokelewa vizuri,” Matthaus alisema.

“Kwasasa kuna mabadiliko yaliyoondoa  uzuri wa soka letu, lakini tunaangalia zaidi kushinda”.
“Katika fainali za Afrika kusini, Ujerumani iliwashangaza wengi kwa soka lao zuri. Hapa Brazil wanacheza soka kwa nguvu, wanatafuta matokeo zaidi”.

Kesho Ujerumani inacheza nusu fainali ya kwanza ya kombe la dunia dhidi ya Wenyeji Brazil na keshokutwa, Uholanzi watachuana na Argentina.

Related Posts:

0 comments: