Monday, 7 July 2014

OFFICIAL: PRANDELLI ATHIBITISHWA KUWA KOCHA WA GALATASARAY, MOYES ATOSWA MCHANA KWEUPE!

Official: Prandelli confirmed as Galatasaray boss


CESARE Prandelli amethibitishwa kuwa kocha mkuu wa klabu ya Galatasaray ya Uturuki zikiwa zimepita wiki mbili tangu ajiuzulu kuifundisha timu ya Taifa ya Italia kutokana na matokeo mabaya ya kombe la dunia nchini Brazil.
Miamba hiyo ya Uturuki imeweka taarifa rasmi kwenye mtandao wao wa klabu leo jumatatu, ikisema kuwa kocha huyo mwenye miaka 56 atasaini mkataba wa miaka miwili kurithi mikoba ya Roberto Mancini.
Prandelli atawasili Uturuki leo jioni kabla ya kusaini mkataba,  na kesho jumanne atatembelea uwanja wa mazeozi pamoja na wachezaji.
Galatasaray walikuwa wakihusishwa kuzungumza na Prandelli tangu ajiuzulu kuifundisha Italia, huku David Moyes naye akihusishwa.
Prandelli atamrithi Mancini katika dimba la Turk Telekom Arena kufuatia kocha huyo kuondoka kwa makubaliano maalum mwezi juni ikiwa ni miezi tisa tangu aanze kazi hiyo.
Mkurugenzi wa michezo wa Galatasaray, Tomas Ujfalusi, siku za karibuni alikiri kuwa ujuzi na uzoefu wa Prandelli katika soka la Italia utasaidia kuendeleza kazi aliyofanya Mancini klabuni hapo.

“Wakati Mancini anasema hataki kuendelea, nilataka kumleya Cesare,” Ujfalusi alikaririwa akizungumza na gazeti la Gazetta dello Sport.

Related Posts:

0 comments: