GWIJI
wa Argentina, Diego Maradona anaamini ndoto za taifa lake kutinga fainali ya kombe
la dunia dhidi ya Uholanzi leo hii zimebebwa mabegani kwa Lionel Messi.
Maradona
amesema wanashukuru kwasababu wana mshambuliaji wa Barcelona ambaye amewapa
mafanikio katika mashindano ya mwaka huu.
Messi
amefunga mabao manne katika mechi tano alizocheza katika mashindano ya mwaka
huu na bado ana presha ya kufanya vizuri leo kutokana na majeraha aliyonayo
Angel Di Maria, ila Maradona anajiamini kuwa nyota huyo atafanya vizuri.
“Ni
kwasababu ya Messi ndio maana tumefika hatua ya nne bora kwa mara ya kwanza
tangu mwaka 1990 na bao moja tu litatufanya tufike karibu na malengo yetu.
Lakini haitakuwa rahisi”. Maradona amewaambia Times of India.
“Kila
kitu tunategemea kwa Messsi ambaye atabaki kuwa mchezaji bora bila kujali
matokeo yatayopatikana”.
“Hakuna
mchezaji bora kama Messi. Kwasababu hachezi soka la nyumbani, wengi wanamtazama
kwa kupitai TV”.
“Baada
ya kushindwa kufika robo fainali mwaka 2006 na 2010 na yeye akiwa sehemu ya
kikosi, mwaka huu umeongeza matarajio”.
Kwa
mara ya mwisho, Argentina alishinda kombe la dunia 1986 walipoifunga Ujerumani
Magharibi mabao 3-2 kwenye mechi ya fainali.
0 comments:
Post a Comment