Saturday, 12 July 2014

KOCHA WA ZAMANI YANGA AMTWANGA MKWARA MZITO MARCIO MAXIMO


Kocha mkuu wa Yanga sc, Marcio Maximo (kulia) akiwa na msaidizi wake Leonardo Neiva (kushoto).

 

UJIO wa Marcio Maximo katika klabu ya Yang sc umemvutia beki na kocha wa zamani wa klabu hiyo, Fred Felix Minziro ambaye kwasasa ni kocha mkuu wa JKT Ruvu ya Pwani.
Akizungumza na MPENJA BLOG, Minziro amesema yeye falsafa yake ni kucheza soka la kuvutia, hivyo anaamini atakuwa mpinzani mkubwa wa Maximo.
“Hakuna asiyefahamu kwamba soka langu ni la kuvutia, hakuna asiyefahamu hilo. Na naamini hata kama timu inanifunga, kila mtu anatoka uwanjani akiwa amaridhika . Nahakikisha kwamba soka hili linarudi tena ndani ya JKT, ingawa mwaka huu lisiwe zuri sana, lakini mwakani litakuwa bora zaidi”.
Kuhusu ujio wa Maximo katika klabu ya Yanga, Minziro alisema amefurahishwa sana kwasababu kocha huyo analijua soka la Tanzania na utamaduni wake.
“Mimi nasema ni vizuri, ujio wa Maximo nimeufurahia sana, mkazo ni kwa viongozi wa Yanga. Unajua viongozi wa Yanga mara nyingi wamekuwa sio wakweli, unaweza kuwaambia unahitaji hiki na hiki na wasikutimizie”.
“Lakini kwa Maximo ninvyomfahamu mimi, ni kocha mwenye msimamo. Nadhani viongozi watafika muafaka na kuteleleza matakwa yake”. Alisema Minziro.
Ujio wa Maximo ni changgamoto nzuri kwangu, kwasababu naamini timu ya JKT Ruvu itakutana na kocha huyo katika ligi, itakuwa ni mechi nzuri.Pambano litakuwa zuri sana”.
“Pia kwa upande wa viongozi, nadhani Maximo atawasukuma na kuhakikisha Dar Young Africans wanajenga uwanja mzuri wa mazoezi, nadhani wakati tukiwa na Brandts tulikuwa tunalalamika uwanja wa mazoezi”.

“Naamini Maximo atawabadilisha viongozi wa Yanga, watabadilika,  wataenda kwa mtindo wa kisasa na kuacha kwenda kizamani”. Alihitimisha Minziro mwenye mapenzi na Yanga sc.

                      Na Baraka Mpenja Dar es salaam

Related Posts:

0 comments: