Saturday, 12 July 2014

HIVI HAWA NDIO WANASTAHILI KURITHI MIKOBA YA `MZEE WA WIKI` LUIZ FELIPE SCOLARI?


Guardiola or Mourinho should replace Scolari'
KOCHA wa Sao Paulo inayocheza ligi kuu ya Brazil, Muricy Ramalho amesema Pep Guardiola na Jose Mourinho wanafaa kuwa warithi wa Luiz Felipe Scolari katika nafasi ya ukocha mkuu wa timu ya taifa ya Brazil.
Hatima ya kocha wa sasa wa Brazil imekuwa matatani kufuatia The Selecao kupigwa kipondo cha aibu cha mabao 7-1 dhidi ya Ujerumani katika mchezo wa nusu fainali ya kombe la dunia iliyofanyika Belo Horinzonte jumanne ya wiki hii.
Kuelekea katika mchezo wa mshindi wa tatu baina ya Brazil dhidi ya Uholanzi usiku wa leo, Ramalho, ambaye pia anatajwa na Zico kurithi mikoba ya Scolari, ametaja majina maarufu ambayo anaamini yanaifaa kazi hiyo.
“Mpira uko hapa mpaka sasa, “ kocha huyo mwenye miaka 58 amewaambia ESPN Brasil.
“Wakati umefika na nadhani kocha wa zamani wa Corinthians, Tite anastahili . Ameshinda makombe mengi. Lazima awe katika orodha ya watakaotajwa”.
“Kama sio Mbarazil, itakuwa vizuri zaidi. Guardiola atakuwa chaguo langu la kwanza. Au Mourinho. Tunatakiwa kuwa na makocha wa kiwanggo cha juu, ambao wana soko hata kibiashara. Watendaji wazuri wa kazi”.
“Kati ya hao wawili, naweza kusema Guardiola. Lakini itakuwa juu ya CBF (shirikisho la soka la Brazil) kuamua. Haya ni maoni yangu na nayaweka wazi”.
Ramalho alikuwa na nafasi ya kuwa kocha wa Brazil mwaka 2010, lakini aliendelea kubaki Fluminense na anasema hajutii kukosa nafasi hiyo na wala hana mpango wa kuomba.

“Mimi sina uchu wa madaraka”. Alisema.

Related Posts:

0 comments: