UHAMISHO wa Wachezaji huko England umeendelea kupamba moto na zifuatazo ni habari zake mpya.
SOMA ZAIDI:
ARSENAL YAMSAINI MATHIEU DEBUCHY TOKA NEWCASTLE UNITED
Arsenal imemsaini Fulbeki Mathieu Debuchy kutoka Newcastle.
Debuchy, Miaka 28, alikuwa mmoja wa Wachezaji wa France waliocheza Kombe la Dunia huko Brazil na ameletwa Emirates kuchukua nafasi ya Bacary Sagna ambae amejiunga na Manchester City kama Mchezaji Huru.
Debuchy, ambae ameigharimu Arsenal Pauni Milioni 12, anakuwa Mchezaji wa Pili kusainiwa na Arsenal kwa Msimu mpya baada kumchukua Alexis Sánchez kutoka Barcelona.
Mfaransa huyo aliichezea Newcastle Mechi 46 katika Miezi 18 aliyokuwa kuwa huko baada kuhamia kutoka Lille ya France ambayo alifanikiwa kutwaa nayo Ubingwa wa Ligue 1 na Coupe de France Msimu wa 2010/11.
JANMAAT ASAINI NEWCASTLE
Newcastle United wamemsaini Fulbeki wa Kimataifa wa Netherlands Daryl Janmaat kutoka Feyenoord kwa Dau ambalo halikutajwa.
Janmaat, Miaka 24, amesaini Mkataba wa Miaka 6 na amenunuliwa ili kuziba pengo la Mathieu Debuchy aliehamia Arsenal
Janmaat aliichezea Netherlands Mechi 5 huko Brazil kwenye Fainali za Kombe la Dunia na kufika nayo Nusu Fainali.
Mdachi huyo alianzia Soka lake huko ADO Den Haag kisha kujiunga na Heerenveen Mwaka 2008 ambako alicheza Mechi zaidi ya 100 kabla kujiunga na Feyenoord Mwaka 2012.
DEMBA BA AFUZU AFYA HUKO BESIKTAS
Straika wa Chelsea Demba Ba amefuzu upimwaji afya huko Besiktas na Ijumaa anatarajiwa kukamilisha Uhamisho wa Pauni Milioni 8.
Ba, mwenye Miaka 29, alianza Mechi 23 kati ya 50 alizochezea Chelsea Msimu uliopita na kufunga Bao 14.
Kwenye Msimu huo, Ba alikuwa nyuma kwa namba akiwa chaguo la mwisho baada ya Samuel Eto'o na Fernando Torres.
Lakini Eto’o hivi sasa amemaliza Mkataba na Chelsea wamemsaini Diego Costa na hivyo Ba kuonekana hahitaji tena.
RIO FERDINAND AFUZU AFYA QPR!
Beki mkongwe Rio Ferdinand anatarajiwa kukamilisha Uhamisho wake kwenda QPR kama Mchezaji Huru baada ya kufuzu upimwaji Afya yake.
Rio, mwenye Miaka 35, ni Mchezaji Huru baada ya kumaliza Mkataba wake na Manchester United alikodumu kwa Miaka 12.
Huko QPR, Rio ataungana tena na Meneja Harry Redknapp ambae ndie alimwibua na kumpa namba kwa mara ya kwanza kama Mchezaji wa Kulipwa walipokuwa wote huko West Ham Mwaka 1996.
Rio anatarajiwa kuwa ndie Mchezaji wa Kwanza kusainiwa na QPR kwa ajili ya Msimu mpya.
SOMA ZAIDI:
ARSENAL YAMSAINI MATHIEU DEBUCHY TOKA NEWCASTLE UNITED
Debuchy, Miaka 28, alikuwa mmoja wa Wachezaji wa France waliocheza Kombe la Dunia huko Brazil na ameletwa Emirates kuchukua nafasi ya Bacary Sagna ambae amejiunga na Manchester City kama Mchezaji Huru.
Debuchy, ambae ameigharimu Arsenal Pauni Milioni 12, anakuwa Mchezaji wa Pili kusainiwa na Arsenal kwa Msimu mpya baada kumchukua Alexis Sánchez kutoka Barcelona.
Mfaransa huyo aliichezea Newcastle Mechi 46 katika Miezi 18 aliyokuwa kuwa huko baada kuhamia kutoka Lille ya France ambayo alifanikiwa kutwaa nayo Ubingwa wa Ligue 1 na Coupe de France Msimu wa 2010/11.
JANMAAT ASAINI NEWCASTLE
Newcastle United wamemsaini Fulbeki wa Kimataifa wa Netherlands Daryl Janmaat kutoka Feyenoord kwa Dau ambalo halikutajwa.
Janmaat, Miaka 24, amesaini Mkataba wa Miaka 6 na amenunuliwa ili kuziba pengo la Mathieu Debuchy aliehamia Arsenal
Janmaat aliichezea Netherlands Mechi 5 huko Brazil kwenye Fainali za Kombe la Dunia na kufika nayo Nusu Fainali.
Mdachi huyo alianzia Soka lake huko ADO Den Haag kisha kujiunga na Heerenveen Mwaka 2008 ambako alicheza Mechi zaidi ya 100 kabla kujiunga na Feyenoord Mwaka 2012.
DEMBA BA AFUZU AFYA HUKO BESIKTAS
Straika wa Chelsea Demba Ba amefuzu upimwaji afya huko Besiktas na Ijumaa anatarajiwa kukamilisha Uhamisho wa Pauni Milioni 8.
Ba, mwenye Miaka 29, alianza Mechi 23 kati ya 50 alizochezea Chelsea Msimu uliopita na kufunga Bao 14.
Kwenye Msimu huo, Ba alikuwa nyuma kwa namba akiwa chaguo la mwisho baada ya Samuel Eto'o na Fernando Torres.
Lakini Eto’o hivi sasa amemaliza Mkataba na Chelsea wamemsaini Diego Costa na hivyo Ba kuonekana hahitaji tena.
RIO FERDINAND AFUZU AFYA QPR!
Beki mkongwe Rio Ferdinand anatarajiwa kukamilisha Uhamisho wake kwenda QPR kama Mchezaji Huru baada ya kufuzu upimwaji Afya yake.
Rio, mwenye Miaka 35, ni Mchezaji Huru baada ya kumaliza Mkataba wake na Manchester United alikodumu kwa Miaka 12.
Huko QPR, Rio ataungana tena na Meneja Harry Redknapp ambae ndie alimwibua na kumpa namba kwa mara ya kwanza kama Mchezaji wa Kulipwa walipokuwa wote huko West Ham Mwaka 1996.
Rio anatarajiwa kuwa ndie Mchezaji wa Kwanza kusainiwa na QPR kwa ajili ya Msimu mpya.
0 comments:
Post a Comment