MWAMBUSI APANIA MAKUBWA ZAIDI MSIMU UJAO LIGI KUU
ZIKIWA zimebaki siku sita kabla ya dirisha la usajili kufungwa, benchi la ufundi la Mbeya City limesema liko katika mikakati mikali ya kusajili wachezaji katika nafasi ya kiungo.
Kocha
wa Mbeya City, Juma Mwambusi amesema yuko katika hatua za mwisho
kukamilisha usajili wa viungo wazoefu kabla dirisha la usajili
halijafungwa rasmi Julai 15.
Mwambusi
ambaye ni kocha bora wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) msimu
huu, amesema kikosi chake hakijaingia kambini Julai 15 kujiandaa kwa
msimu ujao wa ligi hiyo.
"Tumefanya
usajili wa safu ya ushambuliaji na sasa tatizo tunalo kwenye safu ya
kiungo. Tunao viungo wazuri wa kikosi cha kwanza lakini hatuna viungo wa
akiba. Kufikia Julai 14 tutakuwa tumeshapata wachezaji wa nafasi hiyo
maana tayari tuko katika mazungumzo ya mwisho na wachezaji hao," amesema
Mwambusi huku akibainisha kuwa viungo hao wanatoka ndani ya mipaka ya
Tanzania.
"Tutaingia
kambini rasmi Julai 15 lakini bado sijajua tutaweka kambi yetu maeneo
gani maana kuna sehemu tatu ambazo zimependekezwa. Kufikia Julai 14
nitakuwa nimeshachagua mahali pa kwenda," amesema zaidi Mwambusi.
Amesema
kambi hiyo itakuwa ndani ya mipaka ya Tanzania kwa kuwa klabu hiyo
haina utaratibu wa kuweka kambi na kusajili wachezaji wa nje ya nchi.
Hata hivyo, kocha huyo hakuwa tayari kuyaweka wazi maeneo ambayo uongozi
wa timu hiyo umependekeza kwa ajili ya kambi ya timu yake.
Ikiwa
chini ya Mwambusi, huku ikishiriki kwa mara ya kwanza VPL, Mbeya City
imemaliza nafasi ya tatu msimu huu ikizidiwa kete na mabingwa wapya Azam
FC na waliokuwa mabingwa watetezi, Yanga waliokamata nafasi ya pili.
Mbeya City tayari imeshamnasa straika hatari Themi Felix kutoka kwa wakatamiwa wa Kagera, Kagera Sugar.
![]() |
Juma Mwambusi ameelezea mikakati ya Mbeya City msimu ujao |
Na Renatus Mahima, DAR ES SALAAM
0 comments:
Post a Comment