>>MARADONA NDIE WA MWISHO KUBAMBWA ‘MADAWA MARUFUKU’ MWAKA 1994!
SOMA ZAIDI:
MAREFA
FIFA imekanusha taarifa kwamba
imewaagiza Marefa wanaochezesha Kombe la Dunia kutotoa Kadi Nyekundu na
Kadi za Njano ili kufanikisha Fainali ziwe za raha zaidi.
Habari hizo zimezuka kutoka huko Germany
ambako, pamoja na Kambi ya Timu yao huko Brazil, wameshika Mabango
kuhusu Marefa kuipendelea Brazil hasa wakijua Leo hii Nchi yao inaivaa
Brazil kwenye Nusu Fainali ya Kombe la Dunia.
Gazeti la Germany, Bild, liliripoti kuwa
Mkuu wa Marefa wa FIFA, Massimo Busacca, amewaagiza Marefa kutotoa Kadi
nyingi ili kuongeza ladha ya Mchezo lakini Msemaji Mkuu wa FIFA, Walter
De Gregorio, amechukizwa na habari hizo.
Amesema: “Hiyo Stori kwamba FIFA ina
mipango ya siri, Marefa kutotoa Kadi za Njano na Nyekundu ili kuongeza
ladha…kwa maneno mengine, FIFA inahatarisha na kukubali Wachezaji kama
Neymar na wengine kuumizwa. Hili halikubaliki.”
Wajerumani hao wameishikia bango Mechi
ya Brazil na Colombia, ambayo Neymar aliumizwa vibaya na kumfanya akose
Mechi zilizobaki za Kombe la Dunia, kwamba ndio Mechi iliyokuwa na Rafu
nyingi, Rafu 31, na kuzidi Mechi nyingine zote za Fainali za Kombe la
Dunia tangu Mwaka 1966 Takwimu zilipoanza kukusanywa.
Pia, Takwimu zimeonyesha Wastani wa Kadi
za Manjano za Fainali hizi ni 2.8 kwa Mechi ukilinganisha na 3.8
Fainali za 2010 na 4.8 zile za 2006.
De Gregorio amesema: “Hiyo ni sehemu ya
mchezo na tunaikubali. Lakini tusichokubali ni swali la maadili, kwamba
kuna njama za FIFA! Hilo linaingia kabisa kwenye chimbuko la FIFA..la
kuwalinda wahusika wakuu, Wachezaji, ambacho ni kitu muhimu kabisa
kupita yote!”
Aliongeza: “Lazima tulinde Wachezaji. Ikiwa Neymar hachezi Nusu Fainali au Fainali, hii sio nzuri kwetu!”
FIFA- WACHEZAJI SAFI ‘MADAWA MARUFUKU’
FIFA imetoboa kuwa kila Mchezaji
aliepimwa utumiaji ‘Madawa Marufuku’ amekutwa safi baada ya Vipimo zaidi
ya 1,000 kuchukuliwa kwenye Fainali za Kombe la Dunia huko Brazil.
Taarifa hizo zimetangazwa na Kamati ya Afya ya FIFA huko Brazil hapo Jana.
Jiri Dvorak, Daktari Mkuu wa FIFA,
amewaambia Wanahabari huko Maracana, Rio de Janeiro hapo Jana, kuwa kila
Mchezaji wa Timu zote 32 zilizoshiriki Fainali za Kombe la Dunia, ikiwa
ni Jumla ya Vipimo 736, alitoa Damu na Mkojo ili zipimwe.
Dvoraka alisema, kati ya Machi Mosi na
Juni 11, kabla Fainali kuanza huko Brazil, walichukua Vipimo 777 vya
Wachezaji pamoja na vingine 232, yaani Vinne toka kila Mechi katika
Mechi 58 za kwanza, baada Mashindano kuanza hapo Juni 12 na vyote
vilitoa majibu kwamba hamna matumizi ya ‘Madawa Marufuku’.
FIFA imetamka kuwa Mechi 4 zilizobaki,
yaani Nusu Fainali mbili, ile ya kugombea Mshindi wa Tatu na Fainali
yenyewe, pia zitafanyiwa Vipimo vya kustukiza kwa kulenga Mchezaji
yeyote na Matokeo kutolewa kabla ya Mechi inayofuata.
Vipimo vyote vya Wachezaji hurushwa
kutoka Brazil na kupelekwa Switzerland kwenye Maabara ya WADA, World
Anti-Doping Agency, Kitengo cha Kupinga Matumizi ya Madawa Marufuku,
kufanyiwa uchunguzi.
Mara ya mwisho kwa Mchezaji kubambwa
akiwa ametumia ‘Madawa Marufuku’ ni kwenye Fainali za Mwaka 1994 huko
USA ambako Staa wa Argentina, Diego Maradona, aligundulika na kufukuzwa
na kufungiwa.
0 comments:
Post a Comment