Saturday, 12 July 2014

KASEJA, BARTHEZ WAKIONA CHA MOTO KUTOKA KWA MZUNGU WA YANGA SC


KOCHA wa mazoezi ya viungo wa Yanga, Mbrazili  Leonardo Neiva, jana Ijumaa aliwafanyisha mazoezi ya maana makipa, Juma Kaseja na Ally Mustapha ‘Barthez’, kiasi cha wawili hao kutikisa vichwa na kukubali muziki wa Kibrazili.
Neiva ambaye ana nguvu za miguu kama mchezaji anayecheza Ligi Kuu, alikuwa akiwapigia makipa hao wa Yanga mashuti makali golini akilenga katika kingo za magoli hayo kitendo ambacho kiliwapeleka mchakamchaka makipa hao na kushindwa kuokoa michomo mingi.
Awali Kaseja na Barthez pamoja na kipa wa kikosi cha vijana cha Yanga, walikuwa wakipewa mafunzo ya kawaida na kocha wa makipa, Juma Pondamali, lakini Neiva aliingilia kati na kumwomba Pondamali awape funzo la maana makipa hao.

Akizungumza na Mwanaspoti mara baada ya kumalizika kwa mazoezi hayo, Neiva alisema: “Nimejitahidi kuwapigia mashuti japo sijaweza sana kutokana na maumivu ya goti, nashukuru Kaseja na Barthez wanaonyesha mwelekeo, si rahisi kudaka mashuti yote lakini wamefanya vizuri.”
Chanzo: Mwanaspoti

Related Posts:

0 comments: