Thursday, 10 July 2014

EZEKIEL KAMWAGA, UKATIBU MKUU SIMBA SC BASI TENA!


Katibu Mkuu wa Simba, Ezekiel Kamwaga, ameamua kuachana na klabu hiyo baada ya kumaliza mkataba wake wa miezi sita aliokuwa akiutumikia klabuni hapo.

Kamwaga aliingia Simba akiwa katibu mkuu wakati wa utawala wa mwenyekiti Ismail Aden Rage na sasa mkataba wake umemalizika.
Kamwaga, awali alikuwa msemaji wa klabu hiyo kabla ya mkataba wake kumalizika mwishoni mwa mwaka jana, ndipo Rage akampandisha cheo na kuwa katibu mkuu.

Chanzo kutoka ndani ya Klabu ya Simba kilieleza kuwa, katibu huyo amemaliza muda wake na haijajulikana kama ataongezewa na uongozi mpya au la, lakini mwenyewe ametoa ufafanuzi na kudai kuwa hataongeza.

“Kamwaga amemaliza mkataba wake aliokuwa akiutumikia chini ya Rage na haijajulikana kama uongozi uliokupo madarakani utamuongezea mkataba ama la,” kilisema chanzo hicho.

Kuhusiana na jambo hilo, Kamwaga ambaye kitaaluma ni mwanahabari alikiri kumaliza mkataba Simba:



“Nimemaliza mkataba wangu na sitaongeza mkataba mwingine.”
Chanzo:Jamvi la Habari

Related Posts:

0 comments: