Sunday, 15 June 2014

TTFF YASIMAMISHA UCHAGUZI SIMBA! NA RAGE KUENDELEA KUKALIA KITI

SIMBA YATAKIWA IUNDE KAMATI YA MAADILI KABLA JUNI 30!

 RAGE KUENDELEA KITINI!!
ISMAIL_ADEN_RAGERAIS wa TFF, Jamal Malinzi, ametangaza kusimamishwa Uchaguzi Mkuu wa Simba hadi Klabu hiyo itakapounda Kamati ya Maadili kwa mujibu wa Katiba ya TFF.
Uchaguzi Mkuu Simba ulipangwa kufanyika Juni 29 na uamuzi huu wa TFF uliotangazwa Leo kwenye Mkutano wake na Wanahabari unaitaka Simba kuunda Kamati ya Maadili ifikapo Juni 30 na Kamati hiyo ndio itakayoshughulikia masuala yote ya Maadili kuelekea kwenye Uchaguzi Mkuu.
Uamuzi huu wa TFF unaendelea kumweka Madarakani Mheshimiwa Ismail Aden Rage hadi hapo Uchaguzi utakapofanyika baada ya Katiba yao kurekebishwa na kujumuisha Kamati ya Maadili.
Uchaguzi wa Simba umekumbwa na vuta nikuvute Klabuni hasa baada ya Mgombea Michael Wambura kuenguliwa kugombea Urais na Kamati ya Uchaguzi ya Simba na yeye kukata Rufaa TFF ambako Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF, chini ya Mwenyekiti wake Wakili Julius Lugaziya, ilimpitisha na kuamua aruhusiwe kugombea.
Hivi karibuni, Yanga walipitisha uundwaji wa Kamati ya Maadili ya Klabu yao ili kutii amri ya TFF kwenye Mkutano Mkuu wao huko Bwalo la Polisi –Oysterbay, Jijini Dar es Salaam.
Lakini hatua hiyo ililazimu Mkutano huo kumwongezea muda wa Mwaka mmoja Mwenyekiti wa Klabu hiyo, Yusuf Manji, ili aweze kukamilisha masuala ya marekebisho ya Katiba yao na kujumuisha Kamati ya Maadili na pia kuweza kuandaa Mkutano wa Uchaguzi baada ya Katiba mpya kupitishwa na TFF

Related Posts:

0 comments: