Sunday, 15 June 2014

KUNDI LA KIFO [KUNDI {G] KESHO JUMA TATU-- UJERUMANI NA URENO, RONALDO KUITEKETEZA UJERUMANI?

GERMANY_v_PORTUGAL
JUMATATU Usiku huko Arena Fonte Nova Jijini Salvador Nchini Brazil lile ‘KUNDI la KIFO’, Kundi G la Fainali za Kombe la Dunia, litaanza Mechi zake kwa Germany kuivaa Portugal.
Baadae Usiku huo, huko Estadio das Dunas, Mjini Natal, Ghana itacheza na USA kwenye Mechi ya Pili ya Kundi hilo.
Kwa Wadau wengi Germany v Portugal ndio mpambano wenyewe huku wengi wakitaka kumuona Mchezaji Bora Duniani, Cristiano Ronaldo, akijaribu tena kuibeba Nchi yake kama alivyoifikisha Fainali hizi kwa kuiteketeza ‘Mashine ya Kijerumani’.
Miezi 6 iliyopita Germany ilionekana ndio tishio kubwa Duniani lakini baada ya hapo ikafifia baada ya kukabiliwa na Majeruhi kwa Wachezaji kadhaa muhimu, utata wa Kocha Joachim Löw katika kuteua Wachezaji na hata pia uchezaji hafifu kwenye Mechi za Kirafiki.
Baada ya kuwa Majeruhi kwa kitambo, Kambi ya Germany imethibitisha Kipa wao Manuel Neuer na Nahodha Philipp Lahm wako fiti na wataanza Mechi hii.
Lakini Lahm huenda asichezeshwe Fulbeki ya Kulia kama kawaida yake na badala yeke kucheza Kiungo ili kumpisha Mchezaji mwenye nguvu, Jerome Boateng, kumkabili Ronaldo ambae Kocha wa Portugal, Paulo Bento, humchezesha pembeni Kushoto.
Bila ya wasiwasi, Masentahafu wa Germany watakuwa Per Mertesacker wa Arsenal na Mats Hummels wa Borussia Dortmund na Fulbeki Kushoto atacheza Benedikt Höwedes au Erik Durm.
Kiungo wanatarajiwa kusimama Lahm, Bastian Schweinsteiger na Sami Khedira lakini ikiwa watakosekana basi Toni Kroos na Mesut Ozil wanaweza kuziba pengo huku mbele wakiwepo Lukas Podolski na Mario Goetze.
Kwa upande wa Portugal, bila shaka, tegemezi kubwa ni Cristiano Ronaldo.
Kipa, bila mjadala, ataanza Eduardo na Masentahafu ni Bruno Alves na Pepe huku Fabio Coentrao akicheza Fulbeki ya Kushoto na Kulia ni Joao Pereira.
Kocha Paulo Bento, Siku zote hupenda Kiungo ya Mtu 3 na hao ni Raul Meireles, Joao Moutinho na Miguel Veloso ingawa William Carvalho yupo tayari kuchukua nafasi ya yeyote atakaekosekana.
Fowadi ya Portugal itakuwa na Nani upande wa kulia, au Silvestre Varela, kati ni Hugo Almeida na Kushoto ni Ronaldo.
VIKOSI VINATARAJIWA:
PORTUGAL [Mfumo 4-3-3]:
-Eduardo
–Pereira, Alves, Pepe, Coentrao
–Veloso, Meireles, Moutinho
–Nani, Almeida, Ronaldo
GERMANY [Mfumo 4-2-3-1]:
-Neuer
–Boateng, Mertesacker, Hummels, Höwedes
–Lahm, Khedira
–Müller, Özil, Podolski
–Götze
Refa:  Milorad Mazic [Serbia]
KOMBE LA DUNIA
Ratiba:
Saa za  Kibongo
JUMATATU, JUNI 16, 2014
SAA
MECHI
KUNDI
UWANJA
1900
Germany v Portugal
G
Arena Fonte Nova
2200
Iran v Nigeria
F
Arena da Baixada
0100
Ghana v United States
G
Estadio das Dunas
 

Related Posts:

0 comments: