Sunday, 15 June 2014

KOMBE LA DUNIA:HIVI NDIVYO VIKOSI VINAVYO INGIA DIMBANI KATI YA ARGENTINA NA BOSNIA-HERZEGOVINA...MDA MFUPI UJAO:


MESSI_v_DZEKOBAADA Neymar kufungua Akaunti yake ya Magoli ya Fainali za Kombe la Dunia huko Brazil kwa kuweka Bao 2 wakati Brazil inaifunga Croatia Bao 3-1 kwenye Mechi ya Ufunguzi Majuzi Alhamisi, Usiku huu ni zamu ya Supastaa wa Argentina Lionel Messi.
Leo Messi anatinga Estadio Maracana Jijini Rio De Janeiro wakati Argentina itakapoanza kampeni zake kwa kucheza na Bosnia-Herzegovina katika Mechi yao ya kwanza ya Kundi F.
Baada ya kudorora kwa Lionel Messi Miaka minne iliyopita kwenye Fainali za Kombe la Dunia huko Afrika Kusini, Mwaka huu tena mimacho iko kwake kuona nini atafanya.
Lakini Lejendari wa Argentina, Diego Maradona, anamatumaini Staa huyo atawika hasa baada ya ‘kupumzika’ kwa kukosa Mechi nyingi Msimu huu uliokwisha Juzi kutokana na kukabiliwa na Majeruhi.
Maradona ameeleza: “Naona Messi atafanya vizuri. Nadhani ilikuwa vyema kwake kupumzika baada ya kucheza Miaka minne bila kukosa hata Mechi moja.”
Maradona aliongeza: “Ningependa kuongea nae hivi sasa na kumwambia achukulie vitu kiulaini na asiwasikilize Wajinga. Bahati mbaya wako wengi hao!”
Akiielezea Timu ya Argentina kwa ujumla, Maradona ameonyesha wasiwasi wake kuhusu Difensi yao ambao Usiku huu itapambana na Bosnia yenye Wachezaji wasio na mzaha kama vile Edin Dzeko wa Manchester City.
Hata hivyo Safu ya Mashambulizi ya Argentina inampa mchecheto hata Kocha wao Alejandro Sabella na asijue acheze Fomesheni yake anayoipenda ya 5-3-2 au ya Mashambulizi ya 4-3-3.
Lakini, Wachambuzi wa Argentina, waliofuatilia Mazoezi ya Timu hiyo Wiki hii wanahisi Sabella atampiga Benchi Gonzalo Higuain na kuimarisha Safu ya ulinzi na hivyo kutumia 5-3-2 huku mbele wakiwa Aguero na Lavezzi na nyuma yao Messi.
Nae Kocha wa Bosnia, Safet Susic, amesema hawana mpangu kumuwekea Messi Mlinzi maalum.
Ameeleza: “Si vyema kwetu kupoteza Mchezaji mmoja ili amlinde Messi. Hatujawahi kucheza Mechi tukiwa na Mchezaji wetu kazi yake moja tu kumlinda Mtu mmoja na hili halitaanza kwa Argentina!”
Hii ni mara ya kwanza kabisa kwa Bosnia-Herzegovina kucheza Kombe la Dunia kwani ni Nchi changa iliyokuwa huru Mwaka 1995 baada kusambaratika kwa Yugoslavia..
Pamoja na Timu hizi mbili, Timu nyingine Kundi F ni Iran na Nigeria ambazo zitakutana Kesho.
VIKOSI VINATARAJIWA:
ARGENTINA: Romero: Zabaleta, Garay, Fernandez, Rojo; Gago, Mascherano, Maria; Messi, Aguero, Lavezzi.
BOSNIA-HERZEGOVINA: Begovic: Mujdza, Bicakcic, Spahic, Kolasinac; Misimovic, Pjanic, Salihovic, Lulic; Ibisevic, Dzeko.
Refa: Joel AGUILAR [El Salvador]
KOMBE LA DUNIA
Ratiba:
**Saa za Bongo
JUMAPILI, JUNI 15, 2014
SAA MECHI KUNDI UWANJA
1900 Switzerland v Ecuador E Nacional
2200 France v Honduras E Estadio Beira-Rio
0100 Argentina v Bosnia F Estadio do Maracanã
JUMATATU, JUNI 16, 2014
SAA MECHI KUNDI UWANJA
1900 Germany v Portugal G Arena Fonte Nova
2200 Iran v Nigeria F Arena da Baixada
0100 Ghana v United States G Estadio das Dunas
 

Related Posts:

0 comments: