Kitu cha kusikitisha mno kwa Ecuador ni
kuwa kwenye Dakika ya 92, huku Bango likiwa tayari limeashiria Dakika 3
za Nyongeza, Antonio Valencia alichanja mbuga na kuingia ndani ya Boksi
na kumpa Pasi murua Arroyo amalizie tu lakini Mchezaji huyo alifanya
mbwembwe na Mpira kunaswa na Behrami na Uswisi kuanza shambulizi lao la
nguvu ambalo walifunga Bao lao la ushindi.
Bao hilo lilifungwa na Haris Seferovic kwenye Dakika ya 92 na Sekunde 41.
MAGOLI
ECUADOR 1
-Enner Valencia Dakika ya 22
SWITZERLAND 2
-Admir Mehmedi Dakika ya 47
-Haris Seferovic 90 +2:41
Mechi zinazofuata kwa Ecuador ni dhidi ya Honduras Ijumaa Juni 20 wakati Uswisi itacheza na France Siku hiyo hiyo.
VIKOSI:
SWITZERLAND: Benaglio, Lichtsteiner, Rodriguez, Von Bergen, Djourou, Inler, Behrami, Shaqiri, Xhaka, Stocker, Drmic.
ECUADOR: Dominguez, Paredes, Ayovi, Guagua, Erazo, Antonio Valencia, Noboa, Gruezo, Montero, Caicedo, E. Valencia.
Refa: Ravshan IRMATOV [Uzbekistan]
KOMBE LA DUNIA
Ratiba/Matokeo:
**Saa za Bongo
JUMAPILI, JUNI 15, 2014 |
|||
SAA |
MECHI |
KUNDI |
UWANJA |
1900 |
Switzerland 2 Ecuador 1 |
E |
Nacional |
2200 |
France v Honduras |
E |
Estadio Beira-Rio |
0100 |
Argentina v Bosnia |
F |
Estadio do Maracanã |
JUMATATU, JUNI 16, 2014 |
|||
SAA |
MECHI |
KUNDI |
UWANJA |
1900 |
Germany v Portugal |
G |
Arena Fonte Nova |
2200 |
Iran v Nigeria |
F |
Arena da Baixada |
0100 |
Ghana v United States |
G |
Estadio das Dunas |
Hapo jana nayo Ivory Coast yawika Brazil
Ivory Coast ikishambulia lango la Japan
Miamba ya soka barani Afrika
Ivory Coast imeimarisha matumaini ya bara hili baada ya kutoka nyuma na
kuishinda Japan kwa mabao mawili kwa moja.
Ivory Coast ilijipatia mabao yake kupitia
wachezaji Wilfried Bony na aliyekuwa mchezaji wa Arsenal Gervinho huku
Japan ikifunga kupitia mshambuliaji wake keisuke Honda.Ikiwa ni mara ya tatu kwa Ivory Coast kushiriki katika michuano ya Kombe la dunia,haijawahi kufuzu kupitia michuano ya kimakundi.
Hatahivyo chombo kilikuwa chaenda mrama baada ya kocha Sabri Lamouchi kuwashangaza wengi alipomuacha nje aliyekuwa mshambuliaji wa Chelsea Didier Drogba na kusababisha miamba hiyo kuwa chini kwa bao moja ilipofikia kipindi cha mapumziko.
Japan ambayo ndio mabingwa wa bara Asia walikuwa hatari katika ngome ya Ivory Coast kila walipopata mpira na walifanikiwa kupata bao la kwanza katika dakika ya 16 kutoka mshambuliaji wao Honda.
Mchezaji huyo wa kiungo cha kati anayeichezea kilabu ya A.C Milan alipata pasi murwa karibu na lango la upinzani kabla ya kupiga mkwaju mkali uliomuacha mlinda lango wa Ivory Coast kinywa wazi
0 comments:
Post a Comment