Iran
na Nigeria zimetoka 0-0 hapo Jana huko Arena da Baixada Jijini Curitiba
Nchini Brazil katika Mechi ya Kundi F la Fainali za Kombe la Dunia na
hii ndio Droo ya kwanza ya Mashindano haya tangu yaanze Juni 12.
Nigeria walitawala Mpira lakini walishindwa kuipenya Iran inayofundishwa na Kocha wa zamani wa Manchester United Carlos Queiroz.
Nafasi safi za Nigeria zilikuwa Kipindi cha Kwanza wakati Ogenyi Onazi alipopiga nje na Ahmed Musa kukosa kwa Frikiki.
Na nafasi nzuri ya Iran ilikuwa ile ya Reza Ghoochannejad ambayo iliokolewa na Kipa wa Nigeria Vincent Enyeama.
Kwenye Mechi nyingine ya Kundi F iliyochezwa Juzi, Argentina iliifunga Bosnia Bao 2-1.
Mechi zinazofuata za Kundi F ni Jumamoso Jini 21 Argentina v Iran na Nigeria v Bosnia-Herzegovina.
VIKOSI:
IRAN: Haghighi; Montazeri, Hosseini, Sadeghi, Pooladi; Hajsafi, Nekounam, Teymourian, Dejagah; Ghoochannejhad, Heydari.
Akiba: Ahmadi, Shojaei, Haghighi, Reza Jahanbakhsh, Ansarifard, Haddadifa, Mahini, Alenemeh, Rahmani, Beikzadeh, Beitashour, Davari/
NIGERIA: Enyeama; Ambrose, Oboabona, Omerou, Oshaniwa; Mikel, Onazi, Azeez, Moses; Musa, Emenike.
Akiba: Yobo, Uzoenyi, Gabriel, Egwuekwe, Odemwingie, Odunlami, Ejide, Babatunde, Nwofor, Uchebo, Agbim, Ameobi
Refa: Carlos Vera (Ecuador)
KOMBE LA DUNIA
Ratiba/Matokeo:
**Saa za Bongo
JUMATATU, JUNI 16, 2014 |
|||
SAA |
MECHI |
KUNDI |
UWANJA |
1900 |
Germany 4 Portugal 0 |
G |
Arena Fonte Nova |
2200 |
Iran 0 Nigeria 0 |
F |
Arena da Baixada |
0100 |
Ghana 1 United States 2 |
G |
Estadio das Dunas |
JUMANNE, JUNI 17, 2014 |
|||
SAA |
MECHI |
KUNDI |
UWANJA |
1900 |
Belgium v Algeria |
H |
Estadio Mineirão |
2200 |
Brazil v Mexico |
A |
Estadio Castelão |
0100 |
Russia v South Korea |
H |
Arena Pantanal |
0 comments:
Post a Comment