Saturday, 14 June 2014

HIVI NDIYO VIKOSI VITAKAVYO CHEZA MECHI KATI YA ENGLAND V ITALY! MDA MFUPI UJAO

 
 LEO JUMAMOSI, Juni 14, Saa 7 Usiku, Arena Amazônia, Manaus, Brazil
KUNDI D la Fainali za Kombe la Dunia huko Brazil Usiku huu zinaanza Mechi zao za kwanza kwa Uruguay kuivaa Costa Rica huko Estadio Castelão Jijini Fortaleza na kufuatia ule mtanange unaongojewa kwa hamu, England v Italy.
PATA TAARIFA ZA WACHEZAJI/TATHMINI/REKODI/VIKOSI:
Hali za Wachezaji
ENGLAND_v_ITALY_WC2014Fowadi wa England Danny Welbeck amepona tatizo lake la enka lakini Alex Oxlade-Chamberlain bado hajapona maumivu ya Goti lake aliloumia walipocheza Mechi ya Kirafiki na Ecuador huko Marekani Wiki 2 zilizopita.
Italy huenda wakalazimika kutumia Masentahafu wa 3 nyuma badala ya kusimamisha Difensi ya Mtu 4 baada ya Fulbeki wao Mattia De Sciglio kuumia Pajani.
Lakini habari njema kwa Italy ni zile za Mario Balotelli na Marco Verratti kupata afueni matatizo yao kiafya.Arena_Amaznia_Manaus_Brazil
Tathmini
ENGLAND_WC_2014_POSTER-ROONEYMatumaini ya England ya mafanikio kwenye Mechi za Kimataifa yanaanza na Kikosi cha Cesare Prandelli, Italy, ambacho ndicho kilichowatoa kwenye Mashindano ya mwisho makubwa huko kwenye michuano ya EURO 2012 walipobwagwa kwa Mikwaju ya Penati.
Kila Timu inatinga ndani ya Arena Amazônia Jijini Manaus ikihofia athari za Joto na hivyo watacheza Soka la tahadhari la kumiliki Mpira ili wasiupoteze ovyo na kupoteza nguvu ovyo kwa kuukimbiza kutaka kuumiliki tena.
Kama ilivyokuwa kwenye EURO 2012, Mpishi mkuu wa Italy ni Mkongwe Andrea Pirlo, ambae sasa ana Miaka 35, na ambae huko Kiev Miaka minne iliyopita alitoa Pasi nyingi kupita Wacheza wote wa Kiungo wa England na kuzunguka umbali mrefu kupita Mchezaji yeyote wa England kwenye Mechi hiyo ya EURO 2012.
Lakini England ya hivi sasa, chini ya Meneja Roy Hodgson, ni ya Chipukizi wengi, kina Daniel Sturridge, Raheem Sterling na Ross Barkley, wakiongezwa nguvu na Wakongwe Steve Gerrard, Frank Lampard na Wayne Rooney.
Uso kwa Uso
-Jumla Mechi 24
-England: Ushindi Mechi 8 Magoli: 30
-Sare: 7
-Italy: Ushindi 9 Magoli: 27
Dondoo muhimu
-Mara pekee kwa England na Italy kukutana kwenye Kombe la Dunia ni kwenye Mechi ya kuwania Mshindi wa Tatu Mwaka 1990 ambayo Italy walishinda 2-1.
-England wameshinda Mechu 2 tu kati ya 11 walizocheza mwisho dhidi ya Italy wakifungwa 6.
-Mara ya mwisho kukutana ilikuwa huko Switzerland Mwezi Agosti Mwaka 2012 na England kushinda 2-1.
VIKOSI VINAVYOTARAJIWA:
England: Hart, Johnson, Jagielka, Cahill, Baines, Gerrard, Henderson, Lallana, Sterling, Rooney, Sturridge
Italy: Buffon, Abate, De Sciglio, Bonucci, Chiellini, De Rossi, Pirlo, Verratti, Candreva, Marchisio, Balotelli
REFA: Bjorn Kuipers [Holland]
JUMAMOSI, JUNI 14, 2014
SAA
MECHI
KUNDI
UWANJA
REFA
1900
Colombia v Greece
C
Estadio Mineirão
Mark Geiger [USA]
2200
Uruguay v Costa Rica
D
Estadio Castelão
Felix Brych [Germany]
0100
England v Italy
D
Arena Amazonia
Bjorn Kuipers [Holland]
0400
Ivory Coast v Japan
C
Arena Pernambuco
Enrique Osses [Chile]
 

Related Posts:

0 comments: