Friday, 4 July 2014

SUAREZ ANACHEMKA KWENDA BARCA, BORA AENDE REAL MADRID, USHAURI WA PAUL SCHOLES HUO

GWIJI wa Manchester United, Paul Scholes anaamini kwamba mshambuliaji wa Liverpool, Luis Suarez anafanya makosa kutaka kusaini Barcelona. 
Mshambuliaji huyo mtata wa Uruguay anajiandaa kuhamia klabu hiyo ya Katalunya, baada ya Liverpool kuingia majadiliano na viongozi wa Barcelona wiki hii, kufuatia Suarez kufungiwa miezi mine baada ya kumng'ata beki wa Italia, Giorgio Chiellini katika Kombe la Dunia.
Anakwenda kujimaliza? Paul Scholes anaamini kuliko kwenda Barcelona, Luis Suarez bora angeenda Real Madrid
Top dog: Scholes doesn't think that Suarez would play well alongside Barcelona's talisman Lionel Messi
Scholes hafikiri kwamba Suarez atacheza vizuri pamoja na mkali wa mabao wa Barcelona, Lionel Messi

Scholes, pia amehoji kama Suarez ataendana Muargentina Lionel Messi katika kikosi cha Barca na kisha amependekeza mshambuliaji huyo ni bora ahamie Real Madrid.
"Ikiwa Luis Suarez atasaini Barcelona kutoka Liverpool, je Lionel Messi ‘atamkubali yeye? Suarez ni mshambuliaji wa kati na hatataka kucheza pembeni. Sioni namna gani Suarez na Messi watacheza pamoja,". 
"Inasemekana kwangu, ikiwa Messi atakupenda, utacheza. Asipokupenda huwezi, unapoteza muda wako. Na, kwa kweli, nafikiri Suarez anafanya makosa makubwa sana kwenda Barcelona – ni bora angehamia Real Madrid,".

Related Posts:

0 comments: