Thursday, 10 July 2014

NEYMAR KUUNGANA NA BRAZIL KUSAKA NAFASI YA TATU DHIDI YA UHOLANZI


MSHAMBULIAJI majeruhi, Neymar Jr atahudhuria mechi ya mshindi wa tatu siku ya jumamosi kati ya nchi yake ya Brazil dhidi ya Uholanzi.

 Brazil waliomkosa Neymar katika mechi ya nusu fainali dhidi ya Ujerumani na kulala kwa mabao 7-1 watachuana na kikosi cha Louis van Gaal ambao kilitolewa jana kwa mikwaju ya penati 4-2 dhidi ya Argentina.

Neymar aliyeibeba Brazil mechi za nyuma alikosekana na kusababisha nchi yake ifanyiwe kitendo cha `Ukatili` na Wajerumani.

Nyota huyo wa Barcelona alivunjika mfupa wa uti wa mgongo wakati wa mechi ya nusu fainali dhidi ya Colombia nah ii ilitokana na kugongwa kwa goti mgongoni na Juan Zuniga.

“Neymar atakuja hapa (kwenye kikosi cha Brazil). Lengo ni kuwasapoti wachezaji wenzake kwenye mechi ya jumamosi”. Msemaji wa Shirikisho la Brazil, Rodrigo Paiva amethibitisha alipozungumza na R7.com.

Paiva alitangaza taarifa  hizo akiwa makao makuu ya fainali za kombe la dunia, mjini Teresopolis, karibu na Rio de Janeiro.

Hata hivyo, wiki hii madaktari wa klabu ya Barcelona wameripotiwa kumtembelea mshambuliaji huyo wa Barca akiwa nyumbani kwao.

Taarifa kutoka katika mtandao wa klabu ya Barcelona ilisomeka: “Wiki hii Madaktari wa FC Barcelona walimtembelea Neymar Jr akiwa nyumbani kwao nchini Brazil”.

“Viongozi wa CBF na madaktari wa Barca wapo katika makubaliano kujua aina ya matibabu atakayopata ili kuimarika kiafya”.


Kukosekana kwa Neymar  na beki aliyekuwa na adhabu, nahodha Thiago Silva kulichangia kwa kiasi kikubwa kufungwa mabao mengi na Ujerumani ambao watavaana na Argentina siku ya jumapili kwenye mchezo wa fainali wa kombe la dunia.

Related Posts:

0 comments: