
Juma
Mwambusi (wa kwanza kushoto) akiwa na Maka Mwalwisyi (wa pili kushoto)
kwenye moja ya mechi ya Mbeya City fc katika uwanja wa Sokoine jijini
Mbeya.
ALIYEKUWA kocha msaidizi wa Mbeya City fc, Maka Mwalwisyi amedhamiria kupata changamoto mpya katika kazi yake ya ukocha baada ya kuamua kuachana na klabu hiyo kutokana na mkataba wake kumalizika.
Akizungumza
na MTANDAO HUU, Maka amesisitiza kuwa
mara baada ya mkataba wake wa miaka miwili kumalizika tangu mei 30, aliamua
kuhudhuria kozi ya CAF ya leseni B, hivyo anaona kuna haja ya kuachana na kazi
ya kuwa kocha msaidizi wa Juma Mwambusi.
“Baada
ya mkataba wangu kumalizika kulikuwa na kozi ya leseni B ya CAF ambayo ilikuwa
inaendelea jijini Dar es salaam, nimehudhuria ile kozi, mwisho wa siku
nilipomaliza nikatafakari na kuona kwamba kidogo nahitaji changamoto baada ya
kuwa na daraja B”. Alisema Maka.
“Na
nahitaji kuwa na timu yangu ambayo itanipa changamoto kama mwalimu wa daraja B,
kocha Mwambusi ana falsafa yake na mimi nina falsafa yangu, kwa hiyo nahitaji
falsafa yangu ionekane na sio kuwa chini ya kocha Mwambusi”. Aliongeza Maka.
Maka
aliyesaidiana na Mwambusi kuifikisha Mbeya City katika nafasi ya tatu msimu
uliopita alifafanua kuwa hana tatizo na
kiongozi yeyote wala mtu yeyote yule bali ameamua mwenyewe kuondoka katika
klabu hiyo kwani anataka kuonyesha falsafa yake.
kwa
sasa mwalimu huyo mwenye daraja B hajapata klabu yoyote ya kuinoa hapa nchini
na amesema imekuwa ngumu kupata timu kwani watu walikuwa wanajua bado yupo Mbeya
city.
Maka
ni muumini mkubwa wa soka la vijana na hata vijana wengi wanaocheza kikosi cha
pili cha Mbeya City walitokea katika akademi yake ya FOYSA.
Mbali
na kutoa wachezaji hao, pia alitoa wachezaji mbalimbali wanaocheza timu tofauti
tofauti za ligi kuu soka Tanzania bara.
Na
Frank Momanyi, Dar es salaam
0 comments:
Post a Comment