Tuesday, 10 June 2014

MICHAEL WAMBURA ARUDISHWA KUGOMBE SIMBA HUKUMU RASMI KUSOMWA KESHO MCHANA

INGAWA Kamati ya Rufani ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) imesema itatangaza kesho mchana uamuzi wa Rufaa ya Mgombea wa Urais wa Simba SC, Michael Richard Wambura, lakini habari zisizo rasmi zinasema gwiji huyo amerudishwa kwenye mbio za kuwania uongozi wa Wekundu wa Msimbazi. 
Wakili Julius Lugaziya ameuambia mtandao huu jioni hii kwamba; “Tumemaliza, lakini tutakuwa na mkutano kesho mchana kutangaza uamuzi, kwa sasa huwezi kupata habari yoyote, tumekubaliana hivyo, yote yatatajwa kesho,”. 
Ni michael wambura akiwa baadhi ya wanachama wa simba pamoja na mashabiki  picha na maktaba
Majibu kama hayo yametolewa pia na Ofisa Habari na Mawasiliano wa TFF, Boniface Wambura Mgoyo, aliyesema; “Uamuzi kuhusu rufani ya Michael Wambura kupinga kuenguliwa kugombea urais wa Rais utatangazwa kesho (Juni 11 mwaka huu) saa 6 kamili mchana na Mwenyekiti wa Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF, Wakili Julius Lugaziya,”.
Lakini kwa mujibu wa habari za kiuchunguzi ambazo MTANDAO HUU  imezipata ni kwamba baada ya mlolongo wote tangu jana Saa 5:00 asubuhi hoteli ya Courtyad, Upanga, Dar es Salaam hadi jioni ya leo, Wajumbe wa Kamati hiyo waliamua kupiga kura kuamua na Wambura akapata kura tatu kati ya tano za kumkubalia aendelee na mbio za Urais Simba SC. Wambura alikata rufaa TFF akipinga uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi ya Simba SC kumuengua katika kinyang’anyiro cha kuwania urais katika uchaguzi wa klabu hiyo unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi huu. Kamati ya Uchaguzi ya Simba SC chini ya Mwenyekiti Wakili Dk. Damas Ndumbaro ilimuengua Wambura kwa sababu alikiuka Katiba ya klabu hiyo, TFF na FIFA kwa kuipeleka klabu hiyo mahakamani.
 Na Mahmoud Zubeiry, DAR ES SALAAM
 kutoka binzubery blog

Related Posts:

0 comments: