Wednesday 17 September 2014

WENGER KUMSAJI CASILLAS JANUARY WAKATI WA DIRISHA DOGO


Kocha Arsene Wenger ameeleza wazi kuwa ataendelea kumfukuzia kwa kasi kipa Iker Casillas wa Real Madrid wakati wa dirisha dogo la usajili Januari, mwakani.

Tayari Wenger alionyesha nia yake ya kumpata Casillas ambaye amekaa Madrid kwa zaidi ya miaka 14 sasa.
Casillas anaonekana kutokuwa na furaha Madrid na hivi karibuni mashabiki walimzomea.
Lakini Wenger pia anaonekana hafurahii kwa asilimia mia kazi ya kipa wake namba moja Wojciech Szczesny ambaye alikuwa langoni walipochapwa 2-0 na Borussia Dortmund, usiku wa kuamia leo.

Bado haijajulikana kama Madrid itakuwa tayari kumuachia Casillas, lakini Wenger anaonyesha ataendelea kuweka wazi nia yake.

0 comments: