Thursday 18 September 2014

ROBINHO AREJESHWA KIKOSINI BRAZIL KUIVAA ARGENTINA

KOCHA wa Brazil, Dunga amemuita tena kikosini mshambuliajo Robinho jana kwa ajili ya michezo ya kirafiki dhidi ya Argentina na Japan mwezi ujao.

Mshambuliaji huyo aliachwa kwenye kikoi hicho cha Dunga mapema mwezi huu Brazil ilipojipima nguvu na Colombia na Ecuador, lakini baadaye aliongezwa kikosini kufuatia Hulk kuumia.
Brazil itacheza na Argentina Oktoba 11 huko Bird's Nest mjini Beijing na Japan siku tatu baadaye mjini Singapore.

Robinho alikuwa benchi Brazil ikiifunga Columbia 1-0 katika mchezo wa kirafiki Uwanja wa Sun-Life  

KIKOSI CHA BRAZIL....

Makipa: Jefferson (Botafogo), Rafael (Napoli)
Mabeki: Mario Fernandes (CSKA Moscow), Dodo (Inter Milan), Danilo (Porto), Filipe Luis (Chelsea), David Luiz (Paris Saint-Germain), Marquinhos (Paris Saint-Germain), Gil (Corinthians), Miranda (Atletico Madrid)
Viungo: Luiz Gustavo (Wolfsburg), Elias (Corinthians), Fernandinho (Manchester City), Ramires (Chelsea), Willian (Chelsea), Philippe Coutinho (Liverpool), Oscar (Chelsea), Ricardo Goulart (Cruzeiro)
Washambuliaji: Everton Ribeiro (Cruzeiro), Robinho (Santos), Neymar (Barcelona), Diego Tardelli (Atletico Mineiro)

0 comments: