Wednesday, 9 July 2014

ASHITAKIWA KWA KOSA LA KUMPIGA MKEWE James Mwakibinga (27) mkazi wa kijiji cha iwambala kata ya Igawilo Wilayani Mbeya Ameshitakiwa kwa balozi wa mtaa huo baada ya kumpiga mke wake Anaye julikana kwa Jina la Salome Mwaipopo. Akiongea Na Mtandao Huu Bi Salome Mwaipopo amesema kuwa ameamua kumshitaki James kwakuwa ana mpiga mara kwa mara na anamsababishia majeraha ya mwili hali ambayo niunyanyasaji wa kijinsia,pamoja na hayo Bi Salome Mwaipopo ameongeza kuwa amemshitaki kwa Balozi ili apate Barua ya kumpeleka Polisi mumewe kwakuwa amezoea kumnyanyasa bila sababu ya msingi. Aki thibitisha kwa tukio hilo Balozi wa mtaa huo Mapinduzi Mwaipopo amesema Amepokea malala miko hayo kutoka kwa mke wa James anaye daiwa kufanyiwa ukatiri wa kijinsia ,Balozi ameongeza kuwa hua akipokea malala miko kutoka kwa mwanamke huyo mara kwa mara na kumuonya James kutokana na tabia yake hiyo ya kumpiga Mkewe . Hivyo balozi wa mtaa huo ametoa wito kwa wanaume wasiwe na tabia za kuwa nyanyasa wake zao kwa sababu nao wana haki ya kuishi na kufanya maamuzi . Kwaupande wake Samsoni Mwakibinga Ambaye ni mdogo wake na James amesema kuwa wame choshwa na tabia ya kaka yao yakumpiga na kumnyanyasa mke wake bila sababu za msingi ni bora apelekwe polisi wa iliakajifunze tabia. Mwandishi. ASHITAKIWA KWA KOSA LA KUMPIGA MKEWE.




James Mwakibinga (27) mkazi wa kijiji cha iwambala kata ya Igawilo Wilayani Mbeya  Ameshitakiwa kwa balozi wa mtaa huo  baada ya kumpiga mke wake Anaye julikana kwa Jina la Salome Mwaipopo.

                 Akiongea Na Mtandao Huu Bi Salome Mwaipopo amesema kuwa  ameamua kumshitaki  James kwakuwa ana mpiga mara kwa mara na anamsababishia majeraha ya mwili hali ambayo niunyanyasaji wa kijinsia,pamoja na hayo  Bi Salome Mwaipopo ameongeza kuwa amemshitaki kwa Balozi ili apate Barua ya kumpeleka Polisi mumewe  kwakuwa amezoea kumnyanyasa bila sababu ya msingi.

                 Aki thibitisha kwa tukio hilo Balozi wa mtaa huo  Mapinduzi Mwaipopo amesema Amepokea malala miko hayo  kutoka kwa  mke wa James anaye daiwa kufanyiwa ukatiri wa kijinsia ,Balozi ameongeza kuwa hua akipokea malala miko kutoka kwa mwanamke huyo mara kwa mara na kumuonya James kutokana na tabia yake hiyo ya kumpiga Mkewe .

             Hivyo balozi wa mtaa huo ametoa wito   kwa wanaume  wasiwe na tabia za kuwa nyanyasa wake zao kwa sababu nao wana haki ya kuishi na kufanya maamuzi .

Kwaupande wake  Samsoni Mwakibinga Ambaye ni mdogo wake na James amesema kuwa wame choshwa na tabia ya kaka yao yakumpiga na kumnyanyasa mke wake  bila sababu za msingi ni bora apelekwe polisi  wa iliakajifunze tabia. 



                                                                                         Mwandishi.

                      Abdul Marwa Mbeya greenews.blogsport.com

Related Posts:

0 comments: