Thursday, 12 June 2014

WATANZANIA KUNUFAIKA NA SEMINA MAALUM YA UONGOZI BORA

 
pix 5
Mkurugenzi wa Mikono Business Consult Themi Rwegasira akifafanua jambo kwa waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam kuhusu semina maalum ya uongozi bora itakayofanyika katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere  tarehe 13 Juni, pembeni yake wa kwanza kulia ni msemaji wa siku hiyo Brian Tracy,Mkurugenzi mtendaji wa Mikono Business Consult Deogratius Kilawe(katikati) na Azim Jamal msemaji kutoka Canada.
………………………………………………………………….


Wasemaji mashuru  katika masuala ya uongozi bora na maendeleo Bw.Brian Tracy kutoka Marekani na Azim Jamal kutoka Canada wataongoza semina maalum ya uongozi katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere Juni 13 kwa vijana wa Kitanzania.
Wakiongea na waandishi wa habari leo jijini dare s Salaam wataalum hao wemesema ni muhimu kuwepo kwa semina hiyo ambayo itawasaidia vijana katikati uongozi na hivyo kuwa na fursa nzuri ya kuajiriwa katika ngazi za juu badala ya kuwapa wageni nafasi hizo,
“Ni vizuri kuhudhuria semina hii kwasababu kupitia semina hii ina mafunzo mazuri kuhusu uongozi  bora kwa kupata mbinu muhimu za uongozi bora kuanzia ngazi ya kampuni hadi ya Taifa hivyo” alisema Brian
Naye Mkurugenzi Mkuu wa Mikono Business Consult aliongeza kwa kusema semina hii itasaidia kuleta maendeleo katika nchi yetu hususani katika nyanja ya uongozi kwa kuweza v kuwa  na viongozi bora wa baadaye watakaofuata taratibu,kanuni na sheria za uongozi katika sehemu zao za kazi.
“kama ukiangalia katika Makampuni makubwa  na Taasisi  za kifedha utaona kuwa ni watanzania wazawa wachache tu ndio wako katika ngazi za juu za uongozi ambapo asilimia 96 ni wageni na asilimia 4 ndio wazawa  kupitia semina hii itabadilisha  utaratibu kwa kuwa na asilimia kubwa ya wazawa katika uongozi wa juu.” Alisema  Deogratius
Semina hii inawalenga watu wote kutoka katika sekta binafsi, sekta za umma,taasisi za kijamii,makampuni ya umma,viongozi wa Kiserikali pamoja  na wale wote waliokatika uongozi  ili kuweza kujijenga zaidi katika enao la uongozi na kupata matokeo mazuri yenye kuleta maendeleo kwa jamii yetu ya Tanzania.
Vilevili Bw. Brian Tracy ambaye ni mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Kimataifa ya Brian Tracy ambayo inajishughulisha na kutoa mafunzo ya maendelao kwa watu mbalimbali,vilevile ameweza kusaidia makampuni 1000,na kuongea na watu milioni tano katika nchi arobaini duniani,pia ameweza kuandika vitabu 45 katika lugha mbalimbali.
Naye Azim Jamal ni mwanzilishi na mkurugenzi wa Corporate Sufi Worldwide Inc kampuni inayojishughulisha na kusaidia wadau  na makampuni kupata stahiki katika kazi zao,na ni mwandishi wa vitabu mbalimbali vilivyotafsiriwa katika lugha 10.
Habari na Lorietha Laurence-Maelezo

Related Posts:

0 comments: