Saturday 21 November 2015

WASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI KWA KUSAFIRISHA MATENGA YA DAWA ZA KULEVYA MOROGORO

  Watu watatu wanashikiliwa na jeshi la polisi mkoani Morogoro kwa tuhuma za kusafirisha matenga nane ya Dawa za kulevya yenye uzito wa kilogramu 120 yaliyokuwa yakisafirishwa kutoka mkoani Singida kwenda jijini Dar es Salamu kwa ajili ya kusambazwa kwa Mawakala.
Kamanda wa polisi mkoa wa Morogoro Leonardi Paulo amesema tukio hilo limetokea Novemba 21 saa tisa usiku eneo la mikese mizani wakati polisi wakiwa katika opersheni maalumu katika barabara ya Morogoro Dar es Salaam ambapo ameseama watuhumiwa wanahojiwa na Polisi na kwamba baada ya upelelezi kukamili watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma hizo.
 
 

0 comments: