Friday 6 November 2015

FIFA yatangaza magoli 10 bora duniani yanayowania tuzo ya Puskas 2015

   

Puskas Award ni tuzo ambayo ilianzishwa October 20 mwaka 2009 na shirikisho la soka duniani FIFA kwa amri ya Rais wa FIFA Sepp Blatter, tuzo hii uhusisha magoli bora kwa mwaka husika ambapo yatachujwa hadi kufikia moja ambalo mfungaji wake atapewa tuzo ya ufungaji bora kwa mwaka husika.
Usiku wa November 6 shirikisho la soka ulimwenguni FIFA limetangaza magoli 1o bora yaliofungwa kwa mwaka 2015 ila November 30 watachuja na kutangaza magoli bora matatu ambayo January 11 2016 Zurich Uswiss watatangaza goli moja bora na mshindi atapewa tuzo ya ufungaji wa goli bora la dunia, miongoni mwa magoli bora yaliotajwa ni goli la Lionel MessiCarlos Tevez na David Ball.

0 comments: