Tuesday 17 November 2015

Chaguzi ndogo, Madiwani viti maalumu hadharani



TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetangaza nafasi 1393 za vita maalum za madiwani kati ya nafasi 1407 za nafasi hiyo ambapo nafasi 15 hazijatangazwa kutokana na kuwa majimbo nane na kata 34 kutofanyika kwa uchaguzi oktoba 25 mwaka huu.

Akitangaza nafasi hizo jana, Mkurugenzi wa Uchaguzi Ramadhani Kailima alisema kuwa uteuzi huo wa nafasi hizo huzingatia moja ya tatu ya idadi ya kata zilizopo kwenye halmashauri au manspaa ya jiji husika.

Kailima alisema kuwa kwa mujibu wa kifungu cha 35(I)(C)sura ya 287,kifungu cha 19(I)(C) sura ya 288 zikisomwa pamoja na kifungu cha 86A  sura 292 za sheria za serikali za mitaa, Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) ikitwaa jumla ya viti 365,kwa Chadema kutwaa viti 280,CUF viti 79 na NCCR mageuzi kutwaa viti sita ,ambapo Chama cha Mapinduzi CCM ikipata viti 1022, na chama cha ACT-Wazalendo ikitwa viti sita.

“Tuna vitaka vyama vya siasa vituletee majina ya madiwani wao ili kuharakaisha shughuli za mabaraza ya halmashauri ambapo kisheria ni kila baraza likinatakiwa lianze kufanya shughuli zake siku 30 baada ya uchaguzi,”alisema Kailima.

Wakati huo huo Mkuregenzi huyo wa uchaguzi alitaja siku za kufanyika kwa uchaguzi wa majimbo ambao uchaguzi wake uliohairishwa kutokana na kufariki kwa wagombea na sababu nyengine zakisheria.

Alieleza kuwa jimbo la Lushoto na Ulanga Mashariki utafanyika Novemba 22,jimbo la Arusha Mjini na Handeni utafanyika Desemba 13 ambapo jimbo Ludewa na Masasi Mjini utafanyika Desemba 20

0 comments: