Friday 13 November 2015

Ombi Kwa Rais Mstaafu Dr. jakaya Kikwete saoma hapa

Nakumbuka Mkapa baada ya kumaliza muda wake alipotea kabisa kwenye media kwa takriban mwezi nzima hadi tukawa na hamu naye, hii inatoa nafasi kwa rais aliye madarakani kujiamini kujenga confidence, na kutoa nafasi kwa wananchi kumjua vizuri rais wao mpya.

Majuzi uliita waandishi wa habari nyumbani kwako Msoga ukaongea juu ya Taifa stars, TV zinakuonyesha mara nyingi kuliko hata rais.

Juzi ulisahau kumkabidhi JPM kitabu tukakuona sambamba na rais, jana tena umeonekana ukiwa na rais mkihani msiba.

Leo utakuwa uwanja wa taifa sambamba na rais Magufuli tutawaona kwenye TV, dah!

Ombi langu kwa rais wetu mstaafu najua bado una hamu ya kuendelea kuonekana maarufu sawa, lakini muda wako umekwisha mpe nafasi successor wako naye ajulikane.

Kulikuwa hakuna sababu yeyote leo wewe na rais kubanana uwanjani.


Nawasilisha.
chanzo udaku specialy

0 comments: