Saturday 9 August 2014

CLUB YA ASTON VILLA YASAJILI BEKI LA LIVERPOOL


KLABU ya Aston Villa imetangaza kumsajili beki wa Ufaransa, Aly Cissokho kutoka Valencia, na sasa linashughulikia suala la uhamisho wa kimataifa.
Beki huyo wa kushoto mwenye umri wa miaka 26 amekubali mkataba wa miaka minne kuingia kikosi cha Paul Lambert.
Villa imetangaza kwenye akaunti yake ya Twitter, ikisema: "Aly Cissokho amejiunga nasi kwa mkataba wa miaka minne @ValenciaCF, kinachofuata ni uhamisho wa kimataifa,".

Uhamisho: Valencia ilimsajili Cissokho kutoka Lyon kwa Pauni Milioni 5 miaka miwili iliyopita, lakini sasa inaweza kumuuza kwa bei nusu ya hiyo

Cissoko aliyeichezea mechi moja timu ya taifa ya Ufaransa, alijiunga na Liverpool kwa mkopo wa muda mrefu Agosti mwaka jana, lakini akacheza mechi 15 tu za ligi kikosi cha Brendan Rodgers kabla ya kurejea Valencia.
Beki huyo alijiunga na klabu hiyo ya Hispania akitokea Lyon mwaka 2012, wakati pia amechezea timu za Porto, Vitoria Setebal na Gueugnon, alikoanzia soka yake.
Cissokho anaungana na wakali kama Kieran Richardson, Joe Cole na Philippe Senderos katika orodha ya wachezaji wapya Villa Park na usajili wake unaweza kugharimu Pauni Milioni 2.

0 comments: