Wednesday 27 August 2014

ETO'O ASAINI EVERTON KWA MIAKA MIWILI

KLABU ya Everton imetangaza kumsajili mshambuliaji Mcameroon, Samuel Eto'o kwa mkataba wa miaka miwili kama mchezaji huru.
Mpachika mabao huyo mwenye umri wa miaka 33 alitemwa na Chelsea mwishoni mwa msimu uliopita na amejiunga na Toffees kufuatia mango wa kuhamia kwa majirani zao, Liverpool kukwama.
Liverpool ilitaka kumsajili Eto'o iwapo ingemkosa Mario Balotelli, lakini baada ya kumnasa Mtaliani huyo, dili hilo limekufa kifo cha kawaida.
Mshambuliaji huyo wa zamani wa Barcelona ametweet; "Rasmi ni mchezaji wa Everton...!!! Acha niwe tayari kwa matarajio na changamoto mpya!!!'  

Anamwaga wino: Mshambuliaji wa zamani wa Chelsea, Samuel Eto'o akisaini mkataba na Everton

0 comments: