Saturday 23 August 2014

BALOTELLI APOKEWA KWA SHANGWE LIVERPOOL,


KLABU ya Liverpool imemuahidi maslahi mazuri Mario Balotelli ili kuhakikisha mshambuliaji huyo mtata anapiga mzigo wa uhakika Anfield.
Baada ya Liverpool kukubali kutoa Pauni Milioni 16 za ada ya uhamisho kwa AC Milan kumnunua nyota huyo, ilifanya kikao kizito na Mino Raiola, wakala wa mchezaji huyo, Balotelli alikwenda mjini Manchester jana kufanyiwa vipimo vya afya na baadaye akakutana uso kwa uso na kocha wa Liverpool, Brendan Rodgers kwa mara ya kwanza. 
Mamia ya mashabiki wa Liverpool yalimlaki wakati anaondoka kwenye viwanja vya mazoezi, Melwood na hakuna shaka atakapata mapokezi mazuri Anfield. 
Mshambuliaji huyo wa Italia atasaini mkataba wa miaka mitatu, ambao utamfanya awe analipwa Pauni zisizopungua 85,000- au 90,000 kwa wiki. Lakini ameahidiwa marupurupu zaidi iwapo atafanya vizuri kazini. 

Mario anakubalika: Balotelli alikutana na mashabiki née ya viwanja vya Melwood baada ya mazungumzo ya uhamisho wa Pauni Milioni 16 kutoka AC Milan
On the way: Balotelli leaves Melwood training ground after talks on Friday
Balotelli akiondoka Melwood jana baada ya kukamilisha mazungumzo
Friday fun: Hundreds of fans gathered outside training ground to catch a glimpse of Balotelli
Mamia ya mashabiki yalijitokeza kumshangilia Balotelli
Super striker: Balotelli arrives at Melwood for talks after flying from Italy in private jet
Hapa ni wakati Balotelli anawasili Melwood kwa mazungumzo

0 comments: