Thursday 21 August 2014

MKWASA AWAPA WAKONGWE MAMBO SAUDI ARABIA WAWAUE MADRID KESHO



Kocha Charles Boniface Mkwasa ‘Master’ ameendelea na mazoezi akiwa na kikosi chake cha Tanzania Eleven huku akitoa mambo mapya kuhakikisha wanakuwa fiti kabla ya mechi ya kesho dhidi ya wakongwe wa Real Madrid.

Mkwasa ambaye amerejea nchini baada ya klabu ya Al Shaollah FC ya Saudi Arabia kuvunja mkataba dhidi yake.
Kwa kushirikiana na Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ na Fred Minziro ‘Baba Isaya’, wamekuwa wakiendelea na mazoezi kwenye Uwanja wa Karume jijini Dar.
Pamoja na mazoezi hayo, wakongwe hao wataingia kambini leo kwenye hoteli ya kisasa ya Sapphire Court ya jijini Dar es Salaam.
Fungu la kwanza la wakongwe wa Madrid likiongozwa na Luis Figo litatua leo nchini na wengine kesho tayari kwa mechi hiyo ya Jumamosi.

MWAMEJA NA MWANSASU

JULIO AKIONGOZA KIKOSI KAMILI.

MKWASA KAZINI

MANENO 'DENIS LAW'


KUTOKA KUSHOTO; MWANAMTWA, MAO, NYENGE, MONJA NA NSAJIGWA


0 comments: