Saturday 17 May 2014

MAMBO HAYA 10 YAKUZINGATIA TAIFA STARS ILI WAIBUKE NA USHINDI DHIDI YA ZIMBABWE

DSC_45751 
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
Tel: 0712461976
ZIMEBAKI saa chache kuwapokea washambuliaji wawili wa Tanzania wanaocheza soka la kulipwa katika klabu ya TP Mazembe ya nchini demokrasia ya Congo, Mbwana Ally Samatta na Thomas Emmanuel Ulimwengu.
Kuwasili kwa nyota hawa wawili kumefufua matumaini kwa benchi la ufundi na jana kocha mkuu Mart Nooij alisema kuongezeka kwa Samatta na Ulimwengu kumekifanya kikosi chache kiwe na nguvu zaidi katika safu ya ushambuliaji.
Wanandinga hao wa Tanzania jana waliichezea TP Mazembe katika mechi ya kwanza ya makundi ya ligi ya mabingwa barani Afrika dhidi ya El Hilal Omdurani ya Sudan na kupigwa bao 1-0 ugenini.
Licha ya uchovu wa mchezo huo na safari waliyoianza leo asubuhi, haitawazuia kuitumikia timu yao ya taifa ya Tanzania, Taifa stars katika mchezo muhimu wa kesho dhidi ya Zimbabwe.
Taifa stars inahitaji kufunga magoli mengi katika mchezo wa kesho ili kujiweka mazingira mazuri ya kusonga mbele.
Kwa muda mrefu sasa Stars imekuwa ikivurunda, lakini kuja kwa kocha mpya kunawafanya watanzania wawe na hamu ya kufuatilia nini kitatokea.
IMG_0750
Samatta na Ulimwengu watawasili Dar leo mchana
Nooij ameiongoza Stars katika mechi moja tu dhidi ya Malawi kwenye uwanja wa sokoine jijini Mbeya na kutoka suluhu ya bila kufungana, lakini mechi ya kesho ni ya kwanza ya kimashindano kuiongoza timu ya taifa ya Tanzania.
Kila mtu ana hamu kuona mfumo wake wa uchezaji na jinsi atakavyowatumia wachezaji wa Stars ambao jana aliwasifu kuwa na vipaji vikubwa na uzoefu katika mashindano ya kimataifa.
Nooij alisema katika mchezo huo hawatacheza kwa kushindana mithiri ya vita dhidi ya Zimbabwe, bali wataingia na kucheza mpira kama walivyojiandaa.
Ili Taifa stars ifanye vizuri kesho, kuna baadhi ya mambo yanatakiwa kuzingatiwa na wachezaji. Najua wamefundishwa, lakini kilichobaki ni kuyatekeleza kwa nidhamu ya kimpira.
Mosi; Wachezaji wetu watatakiwa kuwa shupavu, kucheza kwa kasi, kuzuia kufungwa, na kucheza kwa weledi mkubwa kwasababu nidhamu ya kimchezo ya wapinzani wao ni kubwa na wana watu wanaoweza kuamua matokeo wakati wowote akiwemo mshambuliaji hatari, Knowledge Musoma.
Kusoma zaidi bofya www.bkmtata.blogspot.com

0 comments: