Sunday 20 March 2016

TBC1 Hawana Pesa ya Kurusha Bunge ila Wana Pesa ya Kumrusha kikao cha mkuu wa mkoa wa Dsm Paul Makonda

Jana nikiwa nyumbani naperuzi peruzi channel zetu zina nini cha mimi kuweza kuangalia, wakati napitapita nikapita na TBC, chaneli yetu ya Taifa. Nakutana na Makonda anahutubia, akili ya mwanzo nikawaza labda Rais Magufuli yuko sehemu na Makonda kaalikwa.

Baadae inapita banner kuwa ni kikao cha Makonda na watendaji wa Halmashauri, dah kinarushwa live televisheni ya taifa. Nadhani tatizo lililopo TBC ni aidha kukosa priorities au kuleta siasa lakini si rasilimali fedha au kubana matumizi kama wanavyotuaminisha.

0 comments: