Saturday 19 March 2016

Maandalizi ya Uchaguzi Visiwani Pemba Yakamilika....CUF yasema haya......



Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), imesema maandalizi ya uchaguzi visiwani Pemba yamekamilika na kuwataka wananchi kujitokeza kesho kupiga kura na kuachana na dhana kuwa kutakuwa na vurugu.

Mwandishi wetu alishuhudia malori saba ya Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) yakipakia vifaa vya uchaguzi katika ofisi ya ZEC Pemba katika tukio lililowafanya baadhi ya wananchi kuacha shughuli zao wakishangaa na wengine wakisema; “sasa shughuli imeanza”.

Ofisa Mdhamini wa ZEC Pemba, Ali Mohammed Dadi alisema wameshapokea karatasi na masanduku ya kupigia kura na fomu mbalimbali. 

Alisema karatasi za uchaguzi wa wawakilishi na madiwani zilianza kusambazwa jana na walitarajia kupokea za urais jana jioni na kuzisambaza leo.

Jana, magari 15 ya polisi aina ya Land Rover yakiwa na askari 10 wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) kila moja, zilionekana zikirandaranda katika mitaa ya Pemba.

“Sisi tunachotaka ni amani tu hao askari waje tu watulinde hakuna mfanya vurugu hapa. Hata wakizagaa mtaani kwetu heri tu ili mradi wasituzuie kufanya shughuli zetu, “alisema Ramadhani Hamisi Omar, mkazi wa Chakechake.

kwa upande wa chama cha wananchi cuf wamesema msimamo wao uko pale na wamewataka wananchi wa zanzibar watulie na wandeleee na shughuli zao kama kawada

0 comments: