Monday 21 March 2016

LIVE TOKA Zanzibar Ulinzi mkali kwa kisubiriwa matokeo ambayo yatatangazwa muda wowote kuanzia hivi sasa


Image captionMatokeo ya uchaguzi wa marudio yanatarajiwa kuanza kutolewa leo
Ulinzi umeimarishwa katika ukumbi ambao matokeo ya uchaguzi mkuu wa marudio visiwani Zanzibar yatatangazwa.
Mbwa wa ulinzi pia wametumika kukagua eneo hilo, ambalo mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar Selim Jecha Selim anatarajiwa kutumia kutangaza matokeo baadaye leo.
Tume hiyo bado haijasema ni saa ngapi matokeo ya kwanza yataanza kutangazwa Ingawa leo jioni kuna dalili zote kuwa matokeo yatatangazwa
Mwenyekiti huyo alitupiwa lawama nyingi na upinzani kwa kufuta matokeo ya uchaguzi wa Oktoba 25.
  •  
Licha ya kususia uchaguzi huu wa marejeo na kusema kuwa si halali, bado chama cha wananchi CUF kiliwekwa katika orodha ya washiriki katika zoezi hilo lililofanyika jana.
CUF Kiliuelezea uchaguzi huo kuwa ni batili.
Ukumbi
Image captionUkumbi utakaotumiwa kutangazia matokeo
Idadi ya waliojitokeza kushiriki uchaguzi huo wa Jumapili ilikuwa ndogo.
Zanzibar ina jumla ya wapiga kura 503,860 waliojiandikisha kupiga kura, kwa mujibu wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar.
Kulikuwa na wagombea 14 kwenye karatasi za kura za kumchagua rais. Majina yao ndiyo haya:
1Khamis Iddi LilaACT-W
2Juma Ali KhatibADA-TADEA
3Hamad Rashid MohamedADC
4Said Soud SaidAFP
5Ali Khatib AliCCK
6Ali Mohamed SheinCCM
7Mohammed Massoud RashidCHAUMMA
8Seif Sharif HamadCUF
9Taibu Mussa JumaDM
10Abdalla Kombo KhamisDP
11Kassim Bakar AlyJAHAZI
12Seif Ali IddiNRA
13Issa Mohammed ZongaSAU
14Hafidh Hassan SuleimanTLP

0 comments: