Monday 21 March 2016

LIVE toka zanzibar Matokeo ya uchaguzi yatangazwa muda huu angalia hapa

 

12:08 Dkt Ali Mohammed Shein atangazwa mshindi wa uchaguzi wa urais Zanzibar akiwa na zaidi ya kura 200,000.
11:57 Mgombea urais wa CCM Dkt Ali Mohammed Shein yumo ukumbini.
11:54 Bw Jecha kwa sasa anatoa hotuba ya kufungua kikao cha kutangazwa kwa matokeo.
11:49 Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) Salim Jecha amewasili ukumbi wa kutangaziwa matokeo. Tume imesema itatangaza matokeo yote muda mfupi ujao.
11:27 Gazeti la Mwananchi linaripoti kwamba mgombea urais wa CCM Dkt Ali Mohamed Shein aongoza matokeo ya awali ya urais majimbo ya Chonga kura 3598, Ziwani (2890), Wawi (4147), Ole (3818), Chake Chake (4551). Matokeo rasmi bado yanasubiriwa.
11:00 Baadhi ya waliowania urais wamefika ukumbini na kuketi. Mmoja wao ni mgombea wa ADC Hamad Rashid.
10:30 Wanahabari, waangalizi na maafisa wengine wa uchaguzi tayari wamo ukumbini wakisubiri kuanza kutangazwa kwa matokeo.
10:20 Kulikuwa na wagombea 14 kwenye karatasi za kura za kumchagua rais. Majina yao ndiyo haya:
1Khamis Iddi LilaACT-W
2Juma Ali KhatibADA-TADEA
3Hamad Rashid MohamedADC
4Said Soud SaidAFP
5Ali Khatib AliCCK
6Ali Mohamed SheinCCM
7Mohammed Massoud RashidCHAUMMA
8Seif Sharif HamadCUF
9Taibu Mussa JumaDM
10Abdalla Kombo KhamisDP
11Kassim Bakar AlyJAHAZI
12Seif Ali IddiNRA
13Issa Mohammed ZongaSAU
14Hafidh Hassan SuleimanTLP
10:15 Ulinzi mkali umewekwa katika ukumbi wa kutangazia matokeo. Mbwa wa ulinzi pia wametumika kukagua eneo hilo, ambalo mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar Selim Jecha Selim anatarajiwa kutumia kutangaza matokeo.
10:00 (Saa za Afrika Mashariki). Hujambo! Matokeo ya mapema ya uchaguzi wa marudio uliofanyika visiwani Zanzibar Jumapili yanatarajiwa kutangazwa leo.
Karibu kwa taarifa za moja kwa moja kuhusu kutangazwa kwa matokeo hayo.

0 comments: