KISA KLABU ILIMTENGA KATIKA BIRTHDAY YAKE
MUSTAKABALI
wa Yaya Toure katika klabu ya Manchester City upo shaken baada ya
wakala wake kuishutumu klabu hiyo bingwa Ligi Kuu England kwa kuidharau
siku ya kuzaliwa ya mchezaji huyo.
Kiungo
huyo wa Ivory Coast, ambaye amebakiza mwaka mmoja katika Mkataba wake
unaomfanya alipwe Pauni 220,000 kwa wiki, imeelezwa amechukiwa na
kitendo cha kutotumiwa salamu za kufurahia miaka 31 ya kuzaliwa kwake.
Wakala
wa Toure, Dimitri Seluk amesema: "Kuna uwezekano mkubwa Yaya akaondoka
majira haya ya joto. Amechukizwa. Kilichotokea katika birthday take
kinamaanisha klabu haimjali. Imethibitika,"amesema.
Maneno mazito: Wakala wa Toure, Dimitri Seluk amesema kuna uwezekano kiungo huyo akaondoka Etihad
"Katika
timu ya kawaida, wachezaji wenzake na klabu angalau wangempa salami za
kumtakia heri. Lakini wakati umeshinda taji na siku mbili baadaye una
pati kubwa kusherehekea taji na hakuna mtu aliyekwenda kumtakia happy
birthday Yaya, nini zaidi unachotaka?
"Ikiwa
mchezaji kama Yaya anakwenda Liverpool nawanashinda ubingwa wa Ligi Kuu
kwa mara ya kwanza ndani ya miaka 24, Yaya atakuwa mzuri
Liverpool,"alisema Seluk.
Amemtolea mfano beki wa zamani wa kimataifa wa Brazil, Roberto Carlos alipewa gari aina ya Bugatti Veyron wakati wa birthday yake na klabu ya Anzhi Makhachkala ya Urusi.
Amemtolea mfano beki wa zamani wa kimataifa wa Brazil, Roberto Carlos alipewa gari aina ya Bugatti Veyron wakati wa birthday yake na klabu ya Anzhi Makhachkala ya Urusi.
Gari iendayo kasi: Mwanasoka mstaafu wa Brazil, Roberto Carlos akiingia kwenye Bugatti Veyron lake
Gari zuri: Seluk amesema Carlos alipewa gari hili na Anzhi Makhachkala katika birthday yake
0 comments:
Post a Comment