Saturday 17 May 2014

BAADA YA KUINUA KOMBE LA FA WENGER ASEMA ANABAKI ARSENAL

KOCHA wa Arsenal, Arsene Wenger ameamua kubaki katika klabu hiyo baada ya kuiongoza Gunners kumaliza ukame wa miaka tisa wa mataji kufuatia kuilaza Hull City mabao 3-2 na kutwaa Kombe la FA usiku huu Uwanja wa Wembley.

Hull iliwavunja nguvu mashabiki wa Gunners kwa mabao mawili ya haraka ya kuongoza ndani ya dakika nane, lakini timu ya Wenger ikazinduka na kusawazisha yote kabla ya Aaron Ramsey kufunga la kuongeza ndani ya dakika 30 za nyongeza.
Wenger amesema kwamba matokeo hayo ya Wembley hapaa shaka yanamfanya ajisikie faraja kubakia Emirates na amethibitisha haondoki. 

Raha imerejea: Lukas Podolski akimwagia bia Wenger baada ya kutwaa Kombe la FA

"Wakati wore nimesema mustakabali wangu hautegemei hili, lakini wakati wore nimesema nilitaka kubaki," alisema Wenger alipoulizwa na ITV kama atabaki, kabla ya kusema , "Ndiyo, nitabaki.'
"Tulitaka kuweka historia usiku huu na kushinda mechi na tumefanya hivyo, hizo ni namna zote - namna ya kuianza fainali ya Kombe na namna ya kuzinduka," alisema Wenger.
Silver service: Wenger lifts the FA Cup much to the delight of his Arsenal players
Furaha tupu: Wenger akiinua Kombe la FA kusherehekea na wachezaji wake
Match winner: Aaron Ramsey scored the crucial goal which saw Arsenal win the FA Cup
Mshindi wa mechi: Aaron Ramsey alifunga bao la ushindi na hapa anasherehekea na Kombe la FA

0 comments: